• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MHITA AFANYA ZIARA KIJIJI CHA ISELA, ATOA MAELEKEZO KUBORESHA USALAMA BARABARANI

Posted on: September 26th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita, @mboni_mhita leo Septemba 26, 2025, ametembelea Kijiji cha Isela kilichopo katika Manispaa ya Shinyanga, kwa lengo la kutoa pole kwa familia zilizopatwa na msiba kufuatia ajali ya gari iliyogonga pikipiki na kusababisha kifo cha mtu mmoja na majeruhi mmoja.

Katika ziara hiyo, Mhe. Mhita ameagiza Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Shinyanga kuhakikisha wanajenga matuta na kuweka taa za barabarani katika eneo hilo ili kupunguza kasi ya magari na kuongeza usalama kwa watumiaji wa barabara, hususan waendesha pikipiki na waenda kwa miguu.

“Nimesikitishwa na ajali hii, lakini tunapaswa kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha tunazuia ajali zinazoweza kuepukika. TANROADS naomba mara moja waanze utekelezaji wa ujenzi wa matuta na taa katika eneo hili,” amesema Mhita.

Kwa upande wake, Muhandisi Fred Kipamila Kaimu Meneja TANROADS mkoani hapa ameahidi kutekeleza agizo hilo kwa haraka, akieleza kuwa taratibu za awali zimeanza kuchukuliwa ili kuhakikisha usalama wa wananchi unaimarika.

Aidha, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro @julius_mtatiro aliwataka wananchi kuepuka matumizi ya vileo barabarani na kuzingatia sheria za usalama, akisisitiza waendesha bodaboda kuhakikisha pikipiki zao zina vifaa vya usalama ikiwemo vioo vya pembeni (side mirrors).

Nao wananchi wa Isela wameishukuru Serikali kwa hatua hiyo, wakisema imekuwa ni kilio chao cha muda mrefu kutokana na ajali za mara kwa mara zinazotokea katika eneo hilo.

Ziara hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali ya Mkoa wa Shinyanga kuhakikisha maisha ya wananchi yanalindwa kwa kuweka mazingira salama, hasa katika maeneo yenye changamoto za miundombinu.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA ARIDHISHWA NA UTOAJI HUDUMA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SHINYANGA.

    September 28, 2025
  • WATENDAJI AMCOS WATAKIWA KUWA WABUNIFU ILI KUONGEZA UZALISHAJI NA THAMANI YA MAZAO YA KIBIASHARA.

    September 27, 2025
  • RC MHITA AITEMBELEA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA, ATOA WITO WA KUWEKEZA KATIKA MAADILI NA ELIMU BORA KWA MTOTO WA KIKE.

    September 27, 2025
  • HALMASHAURI SHINYANGA ZATAKIWA KUTENGA BAJETI KUENDELEZA UTOAJI WA HUDUMA ZA MADAWATI YA USTAWI WA JAMII KATIKA STENDI ZA MABASI

    September 27, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AAGIZA MKANDARASI KUKATWA MILIONI 2 KILA SIKU KWA KUCHELEWESHA BARABARA KAHAMA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa