• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MHITA AIPONGEZA HALMASHAURI YA MSALALA KWA KUTWAA UBINGWA WA MASHINDANO YA SHIMISEMITA.

Posted on: September 19th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita  amepokea kombe la ushindi wa mashindano ya SHIMISEMITA kutoka kwa Timu ya Mpira wa Miguu ya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, ambayo imeibuka bingwa wa mwaka huu baada ya kuifunga Geita DC kwa mikwaju ya penalti 4-2 katika mchezo wa fainali uliofanyika kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Jijini Tanga.

Akizungumza leo Septemba 19, 2025 wakati wa hafla ya mapokezi ya kombe hilo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Mhita ameipongeza timu ya Msalala kwa kuonesha uwezo mkubwa na kuutangaza Mkoa wa Shinyanga katika mashindano hayo ya watumishi wa serikali kutoka halmashauri mbalimbali nchini.

“Tuna kila sababu ya kujivunia mafanikio haya. Ushindi huu ni ishara ya juhudi, nidhamu na mshikamano wa watumishi wetu. Nawapongeza sana Msalala kwa kutuwakilisha vyema na kurudi na heshima hii,” amesema RC Mhita.

Katika hatua nyingine, RC Mhita ameziagiza halmashauri zote mkoani Shinyanga kutenga maeneo maalum ya michezo kwa ajili ya watumishi ili kuendeleza vipaji na kujenga afya kupitia ushiriki wa mashindano mbalimbali kama SHIMISEMITA, SHIMIWI.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, Bi. Rose Manumba, amesema ushindi huo ni matokeo ya maandalizi ya muda mrefu, mshikamano wa timu na sapoti kutoka kwa uongozi.

Amesema kuwa ushindi huo umeongeza ari ya kujiandaa kikamilifu kwa mashindano yajayo kwa lengo la kuutangaza vema mkoa wa Shinyanga na Halmashauri ya Msalala kitaifa.

“Tutaendelea kuwekeza katika maandalizi ya timu na kutoa motisha kwa wachezaji ili tuendelee kuleta heshima kubwa zaidi kwa mkoa wetu,” amesema Manumba.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa