• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MHITA AITEMBELEA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA, ATOA WITO WA KUWEKEZA KATIKA MAADILI NA ELIMU BORA KWA MTOTO WA KIKE.

Posted on: September 27th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita @mboni_mhita Septemba 26, 2025, alifanya ziara katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Shinyanga kwa lengo la kujionea maendeleo ya shule hiyo pamoja na kuzungumza moja kwa moja na walimu na wanafunzi.

Katika ziara hiyo, Mhe. Mhita alipata fursa ya kutembelea miundombinu ya shule hiyo, ikiwa ni pamoja na madarasa, mabweni, maktaba na maeneo ya kujifunzia ili kubaini changamoto zinazowakabili wanafunzi na walimu, na kuona namna ya kuzitatua kwa kushirikiana na wadau wa elimu.

Akizungumza na wanafunzi wa shule hiyo, RC Mhita aliwahimiza kusoma kwa bidii, kuwa na nidhamu na kutambua nafasi yao muhimu kama viongozi wa kesho. Alisisitiza kuwa Serikali inatambua umuhimu wa kumwezesha mtoto wa kike kwa kumpatia mazingira rafiki ya kujifunzia na kujilea.

“Ninyi wasichana mna nafasi kubwa katika maendeleo ya jamii yetu. Elimu ndiyo silaha yenu ya kupambana na changamoto za maisha. Jitahidini, msome kwa bidii, na mjitunze,” alisema Mhe. Mhita.

Kwa upande wa walimu, aliwapongeza kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kulea na kuelimisha watoto wa kike huku akiwaasa kuendelea kuwa walezi bora na mifano ya kuigwa katika jamii.

Ziara hiyo pia ilihusisha mazungumzo ya ana kwa ana kati ya Mkuu wa Mkoa na uongozi wa shule, ambapo walimu walieleza mafanikio na changamoto mbalimbali ikiwemo Samani na uhaba wa vifaa vya kufundishia, kama vile Vitabu vya kiada na ziada na Vifaa vya Kompyuta.

Mhe. Mhita alihitimisha kwa kusema kuwa Serikali ya Mkoa itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha kuwa elimu kwa mtoto wa kike inabaki kuwa kipaumbele, ili kuleta usawa wa kijinsia na kuendeleza maendeleo ya taifa.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa