• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MHITA AMPONGEZA MKANDARASI KWA KASI YA UJENZI WA BARABARA YA KAHAMA–KAKOLA

Posted on: October 3rd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita @mboni_mhita amempongeza mkandarasi wa ujenzi wa barabara ya Kahama Kakola kwa kazi nzuri na kasi ya utekelezaji wa mradi huo muhimu wa miundombinu, ambao unatajwa kuwa kiunganishi muhimu kati ya Mkoa wa Shinyanga na Geita.

Akizungumza hivi karibuni mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 73.1, pamoja na kambi ya kutengeneza malighafi, Mhita alieleza kuridhishwa na hatua iliyofikiwa hadi sasa – ambapo ujenzi umefikia asilimia 45.16.

“Kasi hii inatia moyo. Barabara hii si tu itarahisisha usafiri kwa wakazi wa Kahama, Msalala na maeneo ya jirani, bali pia ni mhimili wa shughuli za kiuchumi, hasa kwa wadau kama Barick ambao hutumia njia hii kusafirisha mitambo na malighafi kwenda Mgodi wa Bulyanhulu,” alisema Mhita.

Aidha, RC Mhita alisisitiza kuwa Serikali ya Mkoa itaendelea kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa mradi huo kuhakikisha unakamilika kwa wakati kama ilivyopangwa.

Kwa upande wake, Meneja wa TANROADS Mkoa wa Shinyanga, Mhandisi Joel Mwambungu, alisema barabara hiyo inajengwa kwa viwango vya kimataifa, ikiwa na upana wa mita 10 hadi 11, huku senta zote zikipangwa kufungwa taa za barabarani kwa ajili ya usalama na uzuri wa miji.

Mradi huu mkubwa wa barabara unatekelezwa kwa gharama ya Shilingi bilioni 106, ukifadhiliwa na kampuni ya Barick kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania. Ujenzi huo unatarajiwa kukamilika rasmi ifikapo Septemba 4, 2026.

Barabara ya Kahama Kakola ikikamilika, itakuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa na kuinua uchumi wa wananchi kupitia biashara, huduma na usafiri wa uhakika.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa