• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MHITA APONGEZA WAHITIMU 81 WA PROGRAMU YA “WANAWAKE NA SAMIA”,ATOA WITO WA KUSHIRIKI UCHAGUZI KWA AMANI

Posted on: October 2nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita @mboni_mhita amepongeza wahitimu 81 wa Programu Maalum ya Wanawake na Samia kwa kukamilisha mafunzo ya miezi miwili ya kuwajengea uwezo wa kiujuzi na kiuchumi, huku akiahidi kuwa serikali itaendelea kuwaunga mkono kupitia fursa za mikopo na miradi mbalimbali ya kimaendeleo.

Akizungumza leo, Oktoba 2, 2025, katika hafla ya mahafali yaliyofanyika katika Chuo cha VETA Shinyanga, Mhe. Mhita alisema serikali ya Mkoa itaendelea kushirikiana kwa karibu na wanawake waliohitimu ili kuhakikisha wanatumia ujuzi waliopata kujitegemea na kuchangia ustawi wa jamii na taifa kwa ujumla.

“Tuna dhamira ya dhati ya kuwawezesha wanawake. Kupitia programu hii, mmepata msingi mzuri wa ujuzi. Ni jukumu lenu sasa kubadilisha maarifa hayo kuwa fursa halisi za kuboresha maisha yenu,” alisema Mhita.

Alitoa wito kwa wahitimu hao kujiunga na vikundi mbalimbali ili waweze kunufaika na mikopo inayotolewa kupitia halmashauri za mkoa huo, mikopo itakayosaidia kukuza uchumi wao kupitia maarifa waliyopata.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Samia, Bi. Futuma Madidi, alitumia fursa hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kwa kuona umuhimu wa kuwawezesha wanawake kiuchumi, huku Mkuu wa VETA Mkoa wa Shinyanga, Bw. Abraham Mbughuni, akieleza kuwa wahitimu hao walipatiwa mafunzo ya vitendo katika fani mbalimbali ikiwemo: saluni, ushonaji, mapishi, madereva, umeme, mapambo, kompyuta na ufundi bomba.

Wahitimu walikabidhiwa vyeti na kuhamasishwa kuanzisha vikundi vya uzalishaji na kutumia stadi walizojifunza kujiletea maendeleo.

Katika kuhitimisha hafla hiyo, RC Mhita aliwasihi wananchi wa Shinyanga kujitokeza kwa wingi kushiriki Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025 kwa amani na utulivu. Alisisitiza kuwa Shinyanga itaendelea kuwa ngome ya utulivu na mshikamano, na kwamba wananchi wasiwe na wasiwasi kwani serikali itahakikisha ulinzi na usalama vinakuwepo siku hiyo.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa