• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MHITA ARIDHISHWA NA UTOAJI HUDUMA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SHINYANGA.

Posted on: September 28th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita @mboni_mhita amefanya ziara ya ukaguzi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga , ambapo amepongeza juhudi za uongozi na watumishi wa hospitali hiyo kwa utoaji mzuri wa huduma kwa wananchi.

Katika ziara hiyo, RC Mhita alipata fursa ya kutembelea wodi mbalimbali zikiwemo wodi za watoto, akina mama, pamoja na maeneo ya maabara, chumba cha upasuaji na huduma za dharura (EMD), ambapo alijionea namna huduma zinavyotolewa kwa weledi na kwa wakati.

“Nimeridhishwa sana na hali ya utoaji huduma katika hospitali yetu ya rufaa. Watumishi wanafanya kazi kwa moyo, mazingira ni safi, na huduma zinatolewa kwa wakati. Hii ni ishara njema kuwa sekta ya afya mkoani Shinyanga inaendelea kuimarika,” amesema RC Mhita.

Aidha, RC Mhita aliwahimiza watumishi wa hospitali hiyo kuendelea kutoa huduma kwa weledi, uadilifu na huruma kwa wagonjwa, huku akisisitiza umuhimu wa usafi, nidhamu ya kazi, na matumizi sahihi ya vifaa na rasilimali zilizopo hususan Vifaa kama CT SCAN ambazo hazikuwepo awali.

Mkuu wa Mkoa pia alipongeza jitihada za Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kuendelea kupeleka vifaa tiba na kuimarisha miundombinu ya hospitali hiyo, hali inayosaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza rufaa za wagonjwa kwenda hospitali za mbali.

Kwa upande wake Mganga mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt Luzila John alieleza kuwa mafanikio yaliyopo yanatokana na ushirikiano mzuri baina ya uongozi wa hospitali, watumishi na Serikali ya Mkoa, huku wakiahidi kuendelea kuboresha huduma zaidi kwa wananchi.

Ziara ya RC Mhita katika hospitali hiyo ni sehemu ya utaratibu wake wa kutembelea taasisi mbalimbali za umma ili kujionea hali halisi ya utoaji wa huduma kwa wananchi na kuhimiza uwajibikaji.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA ARIDHISHWA NA UTOAJI HUDUMA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SHINYANGA.

    September 28, 2025
  • WATENDAJI AMCOS WATAKIWA KUWA WABUNIFU ILI KUONGEZA UZALISHAJI NA THAMANI YA MAZAO YA KIBIASHARA.

    September 27, 2025
  • RC MHITA AITEMBELEA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA, ATOA WITO WA KUWEKEZA KATIKA MAADILI NA ELIMU BORA KWA MTOTO WA KIKE.

    September 27, 2025
  • HALMASHAURI SHINYANGA ZATAKIWA KUTENGA BAJETI KUENDELEZA UTOAJI WA HUDUMA ZA MADAWATI YA USTAWI WA JAMII KATIKA STENDI ZA MABASI

    September 27, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AAGIZA MKANDARASI KUKATWA MILIONI 2 KILA SIKU KWA KUCHELEWESHA BARABARA KAHAMA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa