• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MHITA AWAPOKEA MADAKTARI BINGWA KUTOKA WIZARA YA AFYA – ATOA WITO KWA WANANCHI KUJITOKEZA KWA WINGI KUPATA HUDUMA.

Posted on: October 13th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita @mboni_mhita leo Oktoba 13, 2025, amewapokea rasmi Madaktari Bingwa 36 kutoka Wizara ya Afya waliowasili mkoani humo kwa ajili ya kutoa huduma za kibingwa katika hospitali zote sita za halmashauri za mkoa huo. Huduma hizo zitafanyika kwa muda wa siku tano, kuanzia Oktoba 13 hadi 17, 2025.

Akizungumza katika hafla fupi ya mapokezi iliyofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mhe. Mhita aliwashukuru na kuwakirimu madaktari hao huku akibainisha kuwa ujio wao ni sehemu ya dhamira ya Serikali ya awamu ya Sita kusogeza huduma za afya karibu na wananchi na kupunguza msongamano wa wagonjwa kwenye hospitali za rufaa.

Aliongeza kuwa Serikali ya Mkoa itaendelea kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi ili kufanyiwa uchunguzi, kupewa tiba na ushauri wa kitaalamu kuhusu magonjwa mbalimbali, hususan yale yanayohitaji huduma za kibingwa.

Awali Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga CP Salum Hamdun amesema madaktari hao 36 watahudumu kwenye hospitali za halmashauri sita za mkoa huo na kwamba uwepo wa madaktari hao ni juhudi za serikali za kusogeza huduma kwa wananchi.

Kwa upande wake, Mratibu wa Madaktari Bingwa kutoka Ofisi ya Rais – TAMISEMI Michel Mbele aliwahakikishia viongozi wa Mkoa kuwa timu hiyo imejipanga kutoa huduma bora na za kitaalamu kwa kipindi chote cha siku tano. Amesema lengo ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma stahiki na kwa wakati huku pia wakijenga uwezo wa watumishi wa afya waliopo katika vituo husika.

Huduma zitakazotolewa ni pamoja na magonjwa ya wanawake na uzazi, watoto wachanga, magonjwa ya ndani, huduma za upasuaji, usingizi na ganzi, pamoja na huduma za kinywa na meno.

Mpaka sasa, kupitia mizunguko mitatu iliyopita ya programu hii ya kitaifa, zaidi ya wananchi 230,524 wamenufaika na huduma za kibingwa, huku watumishi wa afya 15,019 wakijengewa uwezo katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwa ni pamoja na Mkoa wa Shinyanga.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa