• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MHITA AZINDUA MPANGO WA KITAIFA WA UGAWAJI WA MBEGU BORA KWA WAKULIMA MSIMU WA 2025/2026

Posted on: October 23rd, 2025

Na Johnson James,  Shinyanga

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, amezindua rasmi Mpango wa Kitaifa wa Ugawaji wa Mbegu Bora kwa Wakulima kwa mpango wa ruzuku kwa msimu wa kilimo 2025/2026, unaolenga kuongeza tija ya uzalishaji, kukuza uchumi wa wakulima na kuongeza pato la Serikali.

Uzinduzi huo umefanyika leo, Oktoba 23, 2025, katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, taasisi za umma na binafsi, wafanyabiashara, pamoja na wakulima wa mazao mchanganyiko kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa huo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mhe. Mhita alisema kuwa kwa msimu wa kilimo wa mwaka 2025/2026, jumla ya tani 192 za mbegu bora za mazao ya choroko, mbaazi, ufuta, dengu na soya zenye thamani ya shilingi bilioni 1.82 zitanunuliwa na kusambazwa nchini kote.

Kwa Mkoa wa Shinyanga pekee, jumla ya tani 3 za mbegu za choroko zitatolewa na kusambazwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Manispaa ya Shinyanga na Halmashauri ya Kishapu ili kuwawezesha wakulima kuongeza uzalishaji na kuboresha kipato chao.

“Ni furaha kubwa kuona mpango huu unatekelezwa kwa vitendo. Tani 192 za mbegu bora zitagawiwa nchini kote, na mkoa wetu utapata tani 3 zitakazowanufaisha wakulima wetu. Hii ni fursa ya kuongeza uzalishaji na kuinua uchumi wa wananchi wetu,” alisema Mhe. Mhita.

Ameeleza kuwa mpango huo ni sehemu ya utekelezaji wa dira ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuhakikisha kilimo kinakuwa uti wa mgongo wa uchumi wa taifa kupitia upatikanaji wa mbegu bora, pembejeo za kilimo na masoko ya uhakika kwa wakulima.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA), Bi. Ireen Mlolwa  alisema mamlaka hiyo inaendelea kuhakikisha wakulima wanapata mbegu zenye ubora na tija, zitakazowawezesha kuzalisha mazao bora yenye soko la uhakika ndani na nje ya nchi.

Bi. Mlolwa aliongeza kuwa COPRA kwa kushirikiana na maafisa ugani na vijana waliopitia programu ya Building a Better Tomorrow (BBT) wataendesha mafunzo ya kuwajengea uwezo wakulima kuhusu mbinu bora za kilimo, matumizi ya mbegu bora na upatikanaji wa masoko yenye faida.

Aidha, aliwahimiza wakulima kujiunga na mifumo rasmi ya stakabadhi ghalani ili kupata fursa ya kuuza mazao yao kwa bei bora na kuepuka hasara zinazotokana na biashara zisizo rasmi.

Kwa ujumla, Mkoa wa Shinyanga umeahidi kuendelea kuboresha sekta ya kilimo kama sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Serikali ya kufanya kilimo kiwe nguzo kuu ya uchumi wa Taifa.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa