• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AIAGIZA TAKUKURU KUCHUNGUZA MRADI WA UJENZI WA KITUO CHA AFYA SALAWE NA KUCHUKUA HATUA STAHIKI

Posted on: November 23rd, 2023

Na. Shinyanga RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina S. Mndeme amekagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga na kubaini uwepo wa uzembe na mianya ya rushwa, na kuwaagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Shinyanga kuchunguza mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Salawe na kuchukua hatua stahiki kwa yeyote atakayekuwa amehusika.

Mhe. Mndeme ametoa agizo hili alipokuwa akifanya majumuisho ya ukaguzi wa miradi inayosimamiwa na Halmashauri, ambapo kwa upande wa Kituo cha Afya Salawe kilipewa zaidi Tzs. Bil. 1 lakini kimeshindwa kumaliza jengo huku kukiwa na malalamiko kutoka kwa wananchi, uongozi wa Kijiji na Kata juu ya uwepo wa hali ya sintofahamu ya utekelezaji wa mradi huku taarifa kuwa mradi umebakiwa na akiba ya Tzs. 1,300/=

"Nawaagiza TAKUKURU muanze kuchunguza mradi huu kuanzia leo hapahapa na atakayebainika achukuliwe hatua stahiki, katika hili nawataka TAKUKURU mchunguze mpaka senti 38 zilizosomwa humu kwenye taarifa yao," alisema Mhe. Mndeme.

"Haiwezekani Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan atoe fedha nyingi kiasi hiki halafu watu wachache tu wazembe, wacheze na fedha hizi na kukwamisha maendeleo kwa wananchi wa kata hii ya Salawe halafu serikali ikae kimya, hiki kitu hakiwezi kuvulimika hata kidogo," alisisitiza Mhe. Mndeme.

Kwa upande wake Diwani Kata ya Salawe Mhe. Joseph Buyugu alimueleza Mhe. Mkuu wa Mkoa kuwa, kumekuwa na ukiukwahi mkubwa sana wa taratibu katika utekelezaji wa mradi huu, kwakuwa ilifika wakati zikavunjwa kamati zote za usimamizi na ufuatiliaji wa mradi na kisha kuundwa nyingine bila ushirikishwaji wowote, hivyo yeye na wengine wakaamua kukaa kando.

Awali Mhe. Mndeme alikagua ujenzi wa jengo la utawala ofisi ya mkurugenzi wa Halmashauri ambapo pia kulibainika uzembe mkubwa sana kwa uongozi wa Menejimenti na mkandarasi amabye ni SUMA JKT kwakuwa ilipelekea fedha kurudishwa serikalini kwa kushindwa kuzitumia kwa wakati. Hivyo akaigiza Halmashauri kufikia Mei, 2024 jengo likamilike na kuanza kutoa huduma kwa wananchi haraka.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa