• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AKUTANA NA WANAWAKE WA KIISLAM MKOA WA SHINYANGA

Posted on: October 4th, 2023

RC MNDEME AKUTANA NA WANAWAKE WA KIISLAM MKOA WA SHINYANGA

Na. Shinyanga RS.MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina S. Mndeme amekutana na Wanawake wa Jumuiya ya Kiislam Shinyanga na kuzungumza nao mambo mbalimbali ikiwemo namna ambavyo serikali ya awamu sita chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania livyoleta fedha zaidi ya Trilioni 1 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika mkoa wa shinyanga.

Mhe. Mndeme amewaeleza kuwa serikali inawajali sana wananchi wa shinyanga ambapo imeboresha zaidi huduma katika sekta ya afya, elimu, maji, miundombinu ya barabara na uwezeshaji wananchi kiuchumi nk.

Aidha Mhe. Mndeme  amewataka kuishi vizuri, kuwajali na kuwafunda watoto wetu wadogo na vijana ili kuzuia mmomonyoko wa maadili, kuepuka na kuacha tabia zisizofaa, zisizofuata maadili na utamaduni wa kitanzania, kukemea na kuzuia kabisa ukatili wa aina yoyote katika maeneo wanayoishi.

Aidha amewaomba kuendelea kumuombea heri na afya njema wakati wote na waendelee kumuunga mkono katika utekelezaji wa majukumu yake ya kuwahudumia wananchi wa shinyanga na tanzania kwa ujumla.

"Ndg zangu akina mama, hakika Rais wetu Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ameifanyia mema mengi na anaendelea kuijali sana shinyanga na hata sasa ninapoongea hapa tumepokea zaidi ya Trioni moja kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa mkoa wetu. Hakika ni kumshukuru sana na tuendelee kumuombea wakati wote ili aifanye kazi ya watanzania bila kuchoka," alisema Mhe. Mndeme.

Akitoa salamu za jumuiya hii Bi. Aisha Juma amesema kuwa, kipekee kabisa na kwa umoja wao wanamuunga mkono na kumuombea kila siku Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ili aendelee, kuwahudumia na kuwaletea maendeleo wananchi wa tanzania, kwakuwa kazi zake wanaziona, wanazikubali na hivyo wanamshukuru sana.

"Tunaendelea kumuunga mkono na kumuombea wakati wote Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili aendelee kuwahudumia na kutuletea maendeleo sisi wananchi wa shinyanga na Tanzania kwa ujumla," alisema Bi. Aisha Juma.

Kando na hayo pia Mhe. Mndeme ameahidi kuchangia mifuko 100 ya saruji kwa ajili ujenzi wa ukumbi wa jumuiya hiyo wilayani Kahama.


HABARI PICHA






Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa