• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AMUAGIZA MRAJIS MSAIDIZI MKOA WA SHINYANGA KUVIFUFUA VYAMA VYA USHIRIKA 12 VILIVYOLALA NA AVIIMARISHE ZAIDI BADALA YA KUANZISHA VINGINE VIPYA

Posted on: September 17th, 2023

Na. Shinyanga RS

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina S. Mndeme amemuagiza Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Shinyanga Bi. Hilda Boniphace kuvifufua vyama vya ushirika 12 vilivyolala kwa kutolipa madeni Benki na aviimarishe badala ya kuanzisha vyama vingine.

Mhe. Mndeme ameyasema haya leo wakati alipokuwa akizungumza na uongozi, watumishi, viongozi wa vyama vya ushirika na baadhi ya wakulima wakati alipofanya ziara katika Chama cha Ushirika Kahama - KACU.

"Nakuagiza Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Shinyanga uvifufue vyama hivi 12 vinavyotajwa kwenye taatifa hii, uviimarishe na kisha uvisimamie kikamilifu viwe na nguvu kama awali na kufanya kazi vvema badala ya kuanzisha vyama vingine vipya," alisema Mhe. Mndeme

Awali kisoma taatifa mbele yake Meneja wq Chama Kikuu cha Ushirika Kahama Ndg. Abdul Ally alimjulisha Mgeni rasmi juu ya uwepo wa Vyama vya Msingi 12 vilishindwa kurejesha madeni ya mikopo ya pembejeo kwenye Benki walizokopa kwa asilimia 100 jambo ambalo lilipelekea kushindwa kuwalipa wakulima wao kutokana na sabahu ya wakulima hao pia kutorosha tumbaku na kwenda kuiuza kwenye vyama vingine.

Kufuatia taarifa hiyo Mhe. Mndeme aliagiza TAKUKURU kufanya uchunguzi wa tuhuma za viongozi na wakulima hao waliotenda hayo na kusababisha deni la zaidi ya Bilioni 2.5 na kwamba watoe taarifa ndani ya siku 30 kuanzia leo tarehe 17 Sept, 2023.

Aidha Mndeme alimuagiza Mrajis Msaidizi kuangalia na kupitia upya mikataba kati ya Vyama vya Msingi, Kampuni zinazonunua Tumbaku na Benki husika ili kuwaondolea mizigo ya madeni wakati inapotokea Kampuni inashindwa kulipa deni hilo jambo ambalo litakwenda kuwaondolea malimbikizo ya madeni wasiyostahili kuyalipa.

KACU LTD imesajiliwa tarehe 20 Aprili, 1994 chini ya Sheria ya Vyama vya Ushirika Na. 15 ya mwaka 1991 fungu la 30 kwa usajili namba 5493 ina wanachama 126 ambapo 36 ni wa zao la Pamba, 46 zao la Tumbaku na 44 wanashughulika na mazao yote mawili.


HABARI NA MATUKIO


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa