• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AWATAKA WAZAZI NA WALEZI KUPELEKA WATOTO SHULE

Posted on: January 8th, 2024

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme amewataka wazazi na walezi wote mkoa wa shinyanga kuhakikisha wanawaleta watoto wao wote ambao wanastahili kusoma kwakuwa hakuna tena ada, kila mtoto anayestahili kusoma atapokelewa na hakuna hata mtoto mmoja atakayebakia nyumbani.

Mndeme ameyasema hayo leo tarehe 8 Januari, 2024 alipotembelea shule ya Awali na Msingi Mwenge, shule ya Sekondari Ngokolo pamoja na shule ya Sekondari Wasichana Shinyanga zote za Manispaa ya Shinyanga ambapo pamoja na mambo mengine pia amewapongeza walimu wote wakiongozwa na Maafisa Elimu wao wote kwa kazi nzuri wanazozifanya ikiwàmo kufundisha, kuhamasisha na kuandisha watoto wapya.

"Nawaomba sana wazazi na walezi wote wenye watoto wanaostahili kusoma muwalete shuleni, hakuna atakayewadai ada, kuwarudishawala hamtapata usumbufu wowote, na hasa wenye ulemavu msiwafiche na kuwaacha nyumbani waleteni shuleni kila kitu ni bure", amesema Mhe. Mndeme.

Kando na wito huo, RC Mndeme amewaeleza wanahabari na walimu waliokuwa katika majumuisho ya ziara hii kuwa, Serikali ya mkoa wa shinyanga imefanikiwa kumuokoa mwanafunzi wa kidato cha kwanza 2024 (jina limehifadhiwa) aliyekuwa ameozeshwa na mzazi wake ajulikanaye kwa jina la Dotto Mjanasa maarufu kama Dullah Mjanasa mkazi wa kijiji cha Iyugi, Kata ya Lyamidati Halmashauri ya Shinyanga amabye alimuozesha kwa jumla ya ng'ombe 15.

Mtoto huyu ambaye amefaulu vizuri sana, amenusuriwa na serikali baada ya wasamalia wema kutoa taarifa a,bapo serikali ilichukua hatua ya harakaya kwenda eneo la tukio na baada ya kumkomboa mzazi huyoa alikimbia  na juhudi za kumtafuta zinaendelea.

Kwa upande wake Afisa Elimu Mkoa wa Shinyanga Mwl. Dafroza Ndalichako amesema kuwa kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi ya 2022, mkoa ulikuwa na maoteo ya kuandikisha wanafunzi wa Awali 75,079 ambapo mpaka sasa wameandikisha wanafunzi 47,182 na kwa darasa la kwanza lengo ni 69,792 huku walioandikishwa ni 44,332 na kwa kidato cha kwanza ni 38,963.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa