• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KITUO CHA AFYA BULIGE - MSALALA

Posted on: September 19th, 2023

Na. Shinyanga RC.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Solomon Mndeme leo tarehe 19 Septemba ametembelea, kukagua na kuweka Jiwe la Msingi ujenzi wa Kituo cha Afya BULIGE kilichopo Halmashauri ya Msalala Wilaya ya Kahama ambapo pamoja na maelekezo mengine lakini pia amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita @mboni_mhita kuhakikisha anasimamia utekelezaji wa maelekezo yake ili kufikia tarehe 30 Oktoba, 2023 ujenzi huo uwe umekamilika na kuanza kutolewa kwa huduma za afya wananchi ambao ni zaidi ya elfu 39.

Akizungumza wakati wa tukio hilo lililojumuisha viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi, Serikali na wananchi Mhe. Mndeme alisema, haiwezekani jambo hili lichukue muda mrefu wakati wananchi wanahitaji kupata huduma na siyo kutazama majengo yaliyojengwa ili tuweze kuwaondolea adha ya kupata huduma hasa akina mama, watoto na wazee ambao ni kundi maalum.

"Nakuagiza Mkuu wa Wilaya Mhe. Mboni kuhakikisha unasimamia maelekezo haya ili ifikapo tarehe 30 Oktoba, 2023 huduma zianze kutolewa hapa ikiwemo Wodi ya kujifungulia akina mama," alisema Mhe. Mndeme.

Kando na maelekezo hayo, pia Mhe. Mndeme ameutaka uongozi wa Kituo hiki kupanda miti kuzunguka eneo lote la Kituo cha Afya kwa ajili ya vivuli, kutunza mazingira na kupendezesha eneo.

Awali akisoma taarifa ya ujenzi wa Zahanati ya Bulige Mganga Mfawidhi Catherine Peter alisema kuwa takribani akina mama 15 hadi 20 hujifungua kila siku katika Zahanati ya Bulige huku akisema kukamilika kwa Kituo hiki kunakwenda kuwa mkombozi wa utoaji huduma katika Kata mbili zenye zaidi ya wakazi elfu 39.

Kata ya Bulige ni moja kati Kata 18 zinazojenga Halmashauri ya Msalala na kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 Kata ya Bulige peke yake ina wakazi 18.184, na ujenzi huu umeanza Februari 2023 na unatarajiwa kukamilika Oktoba 30, 2023 ambapo unakadiriwa kugharimu zaidi ya Milioni 650.

PICHA NA MATUKIO ZIKIMUONESHA MHE. MNDEME AKIKAGUA PAMOJA MKUTANO WA HADHARA AMEONGOZANA NA VIONGOZI MBALIMBALI





Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa