• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AWEKA JIWE LA MSINGI ZAHANATI YA SESEKO, WANANCHI WAMSHUKURU SANA MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

Posted on: September 28th, 2023

RC MNDEME AWEKA JIWELA MSINGI ZAHANATI YA SESEKO, WANANCHI WAMSHUKURU SANA MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

Na. Shinyanga RS

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina S. Mndeme ametembelea, kukagua na kuweka jiwe la msingi katika Zahanati ya Kijiji cha Seseko iliyopo Kata ya Mwamalili Manispaa ya Shinyanga inayohudumia zaidi ya wakazi 2700 iliyoanza kujengwa kwa nguvu za wananchi mwaka 2007 ambapo baadae Serikali imekuja kutoa fedha za kukamilisha ujenzi huu wenye thamani ya zaidi ya Milioni 95 jambo ambalo linawafanya wananchi wa Seseko kumshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuleta fedha hizi na kuwaondolea kero ya kukosa huduma kwa muda mrefu.

Akizungumza baada ya kuweka jiwe la msingi Mhe. Mndeme amewaeleza wananchi hao kuwa, Serikali ya awamu ya sita imeleta fedha hizo katika Zahanati hii kwa lengo la kutatua kero hii ya muda mrefu iliyokuwa ikiwakabili wananchi hawa wakitokea Vitongoji vya Seseko, Nhohola na Ilugala ambapo huduma mbalimbali za afya kwa baba, mama na mtoto zinapatikana sambamba na kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga katika cha Seseko na maeneo jirani kwa ujumla huku akiwataka kuitunza zahanati hii.

"Niwapongeze sana wana Seseko kwa kupata mradi huu wenye kija kubwa zaidi na hatima ya afya zetu, uwepo wa mradi huu unakuja kuondoa kabisa kero ya muda mrefu ya kufuata huduma hii mbali zaidi na sasa Serikali ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuja kuwaondolea kero hii, niwatake sasa niwatake kuitunza zahanati hii ili iwanufaishe na vizazi vijavyo ukizingatia nimekagua na kuona dawa zipo za kutoshq na huduma mnapata zote muhimu," alisema Mhe. Mndeme.

Awali wananchi wa Seseko wakiwa mbele ya Mhe mndeme walitoa Shukurani zao nyingi kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwasaidia kuondokana na kero hiyo ambayo imewasumbua kwa muda mrefu sana, na sasa wanasema hakuna tena kero hii jambo ambalo walimtaka Mhe. Mndeme kuhakikisha anazifikisha shukurani zao kwake Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungajpno wa Tanzania.

Zahanati ya Seseko imesajiliwa na Wizara ya Afyana imeshapata usajili wa MSD, imeanza rasmi kutoa huduma mwezi Agosti, 2023 ambapo huduma zinazoyolewa ni pamoja na huduma za wagonjwa wa nje (OPD), Kliniki ya Baba, Mama na Mtoto, huduma za chanjo pamoja na huduma za upimaji kwa baadhi ya magonjwa.





Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa