• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AZITAKA TAASISI ZINAZOHUSIKA NA UTOAJI WA HAK8 KUFANYA KAZI KWA KUFUATA KANUNI NA SHERIA ZA NCHI

Posted on: January 27th, 2024

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme ameziomba Taasisi zote Mkoani Shinyanga zinazohusika na masuala ya utoaji wa haki kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni na sheria za nchi huku akizikumbusha kufuata maadili ya taaluma zao.

RC MNDEME ameyasema hayo leo tarehe 27 Januari, 2024 alipokuwa akizindua Maadhimisho ya Wiki ya Sheria Nchini ambapo kwa Kanda ya Shinyanga yamefanyika katika viwanja vya Zimamoto vilivyopo Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.

"Naziomba Taasisi zote zinazohusika na masuala ya utoaji wa haki hapa Mkoani Shinyanga mfanye kazi kwa kufuata kanuni na taratibu za nchi na pia kwa mzingatie maadili ya taaluma zenu kwa kufanya hivi mtatoa haki sawa na kwa wakati," amesema Mhe. Mndeme.

Kwa upande wake Mhe. Frank Habibu Mahimbali, Jaji Mfawidhi Mahakama  ya Tanzania Kanda ya Shinyanga amesema kuwa, uwepo wa maadhimisho haya unatoa fursa zaidi kwa wananchi kuhudumiwa kwa ukaribu, kwa wepesi, kwa urahisi na kupata elimu na ufumbuzi wa changamoto mbalimbali zinayowakabili na kutoka kwa watumishi wa Mahakama ambao wamejipanga vema zaidi katika viwanja vya Zimamoto Manispaa ya Shinyanga.

Awali RC MNDEME aliongoza maandamano kutoka Mahakama Kuu kuelekea viwanja vya Zimamoto ambapo pia aliongoza mazoezi ya viungo kwa watumishi na wadau wa Mahakama na mwisho alihitimisha kwa kutoa wito kwa wananchi kujitokeza hapo ili wapate elimu, kutatua kero zao na kushiriki vema maadhimisho haya muhimu kwa ustawi wa Taifa letu.

Maadhimisho haya ya Wiki ya Sheria yamezinduliwa rasmi leo tarehe 27 Januari, 2024 yatahitimishwa tarehe 1 Februari, 2024 yakiwa na Kauli Mbiu isemayo "Umuhimu wa dhana ya haki kwa ustawi wa Taifa: Nafasi ya  Mahakama kwa wadau katika kuboresha Mifumo Jumuishi wa Haki jinai"


HABARI PICHA


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa