• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME MNDEME AFUNGUA MAFUNZO YA WANACHAMA WA KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI WA MIKOA MINNE

Posted on: December 18th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme leo tarehw 18 Desemba, 2023 amefungua mafunzo ya wanachama wa klabu za waandishi wa habari wa mikoa ya Shinyanga, Tabora, Geita na Simiyu kuhusu usambazaji na matumizi ya matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 huku akiwataka wanahabari kutumia elimu na taaluma zao kuelimisha umma juu ya matumizi sahihi ya matokeo ya sensa katika kujiletea maendeleo.

Wito huu umetolewa katika ukumbi wa mikutano uliopo Karena Hotel Manispaa ya Shinyanga ambapo RC Mndeme ameambatana na Kamishna wa Sensa ya Watu na Makazi Mhe. Anna Makinda ambapo pamoja na maelekezo mengine kwa wanahabri lakini ameipongeza sana Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS) kwa kuweza kushirikisha makundi yote katika mchakato huu wa sensa likiwemo kundi la waandishi wa habari ambao amewataja kuwa ni wadau muhimu sana waliofanya kazi kubwa ya kutoa elimu na hamasa kabla, wakati na baada ya zoezi la sensa kwa wananchi.

"Nawapongeza sana Ofisi ya Takwimu ya Taifa na Wanahabari wote kwa kufanya kazi kubwa sana kabla, wakati na hata baada ya zoezi la Sensa ya Watu na Makazi kwa wananchi wetu, jambo ambalo limepelekea kuwa na matokeo chanya kwa serikali hongereni sana", alisema RC Mndeme.

Kwa upande wake Kamishna wa Sensa ya Watu na Makazi Mhe. Anna Makinda aliwaeleza wanahabari kuwa, moja kati ya malengo ya mafunzo haya ni kuwajengea uwezo wanahabari juu ya uelewa wa namna ya kuripoti na umuhimu wa matumizi sahihi ya sensa ikiwa ni pamoja na kuongeza na kuimarisha uwazi katika kuelimisha wananchi.

Awali akitoa taarifa kabla ya kumkaribisha Mtakwimu wa Mkoa wa Shinyanga Ndg. Eliud Kamendu ambaye alimuwakilisha Mtakwimu Mkuu alisema, uwepo wa mafunzo haya ni muhimu sana katika kuwajengea uwezo wanahabari kwenye utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku hasa wanaporipoti taarifa zenye takwimu kama vile za watu na makazi.

Huku DC wa Shinyanga Mhe. Johari Samizi akiwasisitiza wanahabari kuzingatia mafunzo yanatolewa ili yakawe yenye tija katika kazi zao.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa