• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC shinyanga akutana na wamiliki wa shule binafsi

Posted on: September 5th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack, leo tarehe 05/09/2019 amekutana na Wamiliki pamoja na wakuu wa shule binafsi ofisini kwake, kwa lengo la kudumisha mahusiano na kujadili masuala mbalimbali yanayohusu ustawi wa sekta ya elimu Mkoani hapa.

Mhe. Telack akifungua kikao hicho, amesema alikuwa na kiu ya muda mrefu ya kukutana na wamiliki wa shule ili kukaa pamoja na kuona namna bora ya kuongeza ufaulu wa wanafunzi bila kuathiri taaluma na kutoa watoto wanaokubalika kimataifa.

Amesema kasumba ya kuona shule binafsi ni binafsi ni potofu kwani wanaosoma ni watoto wa Watanzania wote.

Amehimiza kuwa, mila potofu zilizopo katika Mkoa wa Shinyanga zitaondoshwa kwa kuhakikisha elimu bora inatolewa katika shule zote zikiwemo shule binafsi.

Aidha, amewataka wakuu wa shule kuwa wakaguzi wa kwanza wa shule zao pale ambapo Wadhibiti ubora hawajafika kutokana na uhaba.

Amewakumbusha pia, wanafunzi wasirudishwe nyumbani kwa kukosa ada hivyo, kila shule iwe na mkataba madhubuti na wazazi ili waweze kulipa ada kwa sababu kumrudisha mtoto ni kuathiri mtiririko wake kitaaluma.

"Wakuu wa shule tumieni taaluma zenu, hakuna mtoto aliyezaliwa akiwa na akili timamu asiyefundishika, badala ya kumfukuza shule wasilianeni na wazazi" amesema Mhe. Telack.

Wakati huo huo, Mhe. Telack amewakumbusha wote kuhakikisha wanashiriki zoezi la uchaguzi wa viongozi wa Serikali za Mitaa kwa kujiandikisha na kupiga kura na kuwamasisha wananchi wengine kushiriki kwani ni kazi ya wote.

Wamiliki pamoja na wakuu wa shule wakitoa maoni na changamoto katika uendeshaji wa shule zao wamehimiza ushirikiano kati yao na Serikali katika masuala mbalimbali ya kitaaluma.

Vilevile, wamemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuitisha kikao hicho na kusema kuwa, kimewapa motisha ya kuendelea kufanya vizuri zaidi ambapo wameomba kiwe ni kikao endelevu kitakachofanyika kila mwanzo wa mwaka kwa lengo la kujipanga kufanya vizuri kitaaluma.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa