• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC Shinyanga amsimamisha kazi Mtendaji wa kijiji cha Nyandekwa

Posted on: February 5th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack ameiagiza Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU Mkoani Shinyanga kufanyia uchunguzi tuhuma zinazomkabili Afisa Mtendaji wa kijiji cha Nyandekwa, Halmashauri ya Mji Kahama Bw. Muhoja Malingumu za kupokea rushwa ili watoto wasiende shuleni.

Telack ametoa agizo hilo leo tarehe 05/02/2020 katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Mji Kahama ambapo amekutana na Watendaji wa kata, Maafisa Elimu kata na Wakuu wa shule za msingi na sekondari wa Halmashauri hiyo, akikamilisha ziara yake ya kukagua shughuli za Elimu Wilaya ya Kahama.

"Baadhi ya Watendaji wanashiriki kula rushwa ili watoto wasiende shule, sasa naanza na Mtendaji wa kijiji cha Nyandekwa, kuanzia leo namsimamisha kazi kwa kutuhumiwa kushiriki watoto wasiende shule, TAKUKURU mfanye uchunguzi. Mtendaji wa kata upo lakini huchukui hatua, humsaidii Mkuu wa shule, wewe pia ukibainika nakusimamisha kazi" amesema Telack akimtaka Mtendaji wa kata hiyo pia Bw. Makoye Kintuki kusimamia maendeleo ya shule.

Telacka amesema haivumiliki kuona baadhi ya watendaji wanajihusisha na vitendo vya rushwa ili watoto wasiende shule.

"Sisi tupo hapa ili watoto wasome, Mhe. Rais anatoa fedha nyingi kila mwezi, hatuwezi kuvumilia kuona vitendo hivi vinafanyika" amesema.

Katika kikao hicho pia, Telack amewahimiza Walimu kufanya kazi za halali za kuwaingizia kipato wakati wa muda wao wa ziada badala ya kutegemea mikopo ya riba kubwa na kuwaletea msongo wa mawazo, hatimaye wanashindwa kufundisha.

Amesisitiza Watendaji wote wanaosimamia Elimu warudi wakasimamie katika maeneo yao ili kuhakikisha ufaulu unapanda.

Bw. Mohamed Kahundi, Afisa Elimu Mkoa amewataka Maafisa Elimu kata kuhakikisha wanazingatia miongozo ya ratiba za vipindi kwenye shule zao.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa