• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC SHINYANGA MH. MBONI MHITA AONGOZA UTATUZI WA MGOGORO WA ARDHI ULIODUMU ZAIDI YA MIAKA 10 KAHAMA

Posted on: September 2nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita ameongoza juhudi za Serikali kutatua mgogoro wa ardhi uliodumu kwa zaidi ya miaka 10 kati ya Chuo cha Maendeleo ya Wananchi (FDC – Mwanva) na wananchi waliokuwa wakiishi ndani ya eneo la hekari 40 zilizotengwa kwa matumizi ya makazi.


Akiwa katika kata ya Malunga, Halmashauri ya Manispaa ya Kahama, Mhe. Mhita alizungumza kwa njia ya simu na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Deogratius Ndejembi, ili kufafanua msimamo wa Serikali kuhusu mgogoro huo ambao awali ulisababisha wananchi kushindwa kuendeleza maeneo yao.


Waziri Ndejembi alieleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan haina nia ya kuwaonea wananchi, na hivyo wale wote waliokuwa ndani ya hekari 40 lakini walisahaulika katika maamuzi ya mwaka 2021 wakati wa uongozi wa Hayati Dkt. John Magufuli, watatambuliwa rasmi na kumilikishwa maeneo yao kihalali.


“Tutawatuma wataalamu kutoka Wizarani wakiongozwa na Kamishna wa Ardhi kwa ajili ya kuwatambua walengwa halali, siyo wale waliovamia baada ya maamuzi ya awali kufanyika. Serikali ipo kwa ajili ya wananchi na haitaki kuona mtu anateseka kwa migogoro inayoweza kutatuliwa,” alieleza Mhe. Ndejembi.


Kwa upande wake, Mhe. Mhita alisema mgogoro huo ameushughulikia kwa muda mrefu tangu akiwa Mkuu wa Wilaya ya Kahama, na sasa juhudi hizo zimezaa matunda baada ya Serikali kutoa mwelekeo sahihi wa kuwatambua ambao walisahaulika kimakosa


Wananchi waliokumbwa na mgogoro huo walitoa shukrani kwa Serikali na kumpongeza Mhe. Mhita kwa kufuatilia suala hilo kwa ukaribu, hali iliyowarejeshea matumaini baada ya miaka mingi ya sintofahamu kuhusu hatma ya maeneo yao.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa