• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC Telack aagiza kukamatwa kwa watakaochanganya mazao

Posted on: January 8th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Taraba kuwakamata wananchi watakaokaidi maelekezo ya wataalamu wa kilimo ya kulima kitalaamu.

Mhe. Telack ametoa agizo hilo akiwa Wilayani Kishapu katika ziara yake ya kukagua shughuli za kilimo na Elimu atakayoifanya kwenye Halmashauri zote Mkoani hapa.

Telack amesema kuwa, Serikali inaposema wakulima wafuate kanuni za kilimo haina maana ya kutaka kuwatesa bali ni kuona kuwa kwa ardhi kidogo wanafaidika na mazao waliyolima.

‘’ Sasa nimesikia kwamba kuna watu wameambiwa limeni kitaalamu hawataki, wanasubiri kukamatwa, ni sawa na mtu anakwambia vaa nguo au kula chakula hutaki” amesema Mhe. Telack.

Amesema Serikali imekuwa na nia thabiti kabisa ya kuwanyanyua wakulima kutoka walipo waende mbele ndiyo sababu ya kuwafukuza maofisini maafisa kilimo na watendaji wa kata kwenda mashambani kusimamia na kuelekeza wakulima na kazi hiyo wameifanya.

Kwa hali hiyo Mhe. Telack amesema wananchi hao wanakaidi amri halali hivyo wakamatwe.

Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za kilimo katika msimu huu, Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Taraba amesema kuwa, Wilaya imelenga kulima hekta 173,257 kwa mazao ya chakula na biashara ambapo lengo ni kuvuna tani 333,380.

Mhe. Taraba amesema kuwa wananchi wamehamasishwa kulima ekari 3 za mazao ya chakula na ekari 3 za mazao ya biashara. Aidha, taasisi kama shule pamoja na watumishi wamehamasishwa kulima pia.

Amesema pia kuwa Wilaya imejiwekea mikakati mbalimbali kuhakikisha Wilaya haipati tatizo la njaa ikiwemo kuwaelimisha wakulima kuhifadhi chakula na kuacha kutumia kwa mahitaji yasiyo ya lazima kama kutengenezea pombe.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa