• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC Telack awashukia wakaguzi wa vyama vya Ushirika

Posted on: October 27th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amewapa siku 2 wakaguzi kutoka shirika la ukaguzi na usimamizi wa vyama vya ushirika COASCO kutoa sababu za kufanya ukaguzi kinyume cha maelekezo ya Ofisi yake katika Chama Kikuu cha Ushirika SHIRECU.

Mhe. Telack amewaagiza wakaguzi hao leo tarehe 27/10/2018 wakati akifungua Mkutano Mkuu wa mwaka wa Chama cha Kurugenzi SACCOS kinachojumuisha Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Manispaa ya Shinyanga.

Akitoa agizo hilo,Mhe. Telack amegeuka mbogo na kusema kuwa COASCO walielekezwa maeneo ya kufanyia ukaguzi katika chama cha SHIRECU na kuwasilisha matokeo ndani ya siku 8, lakini imebainika kuwa SHIRECU imewapatia wakaguzi hao sh. Milioni 20 bila maelezo yoyote na badala yake ukaguzi huo ufanyike kwa siku 25, kitu ambacho ni kinyume na maelekezo ya Ofisi yake.

"Sitaki blabla ndani ya Mkoa wangu, nataka mnipe majibu kwa nini mnafanya ukaguzi kinyume na maelekezo"

Aidha, Mhe. Telack amewataka watumishi ambao ni wanachama wa Kurugenzi SACCOS kutumia chama hicho kwa manufaa yao na kuwekeza ili kujiongezea kipato.

Wakijadili mambo mbalimbali katika mkutano huo,wanachama wameutaka uongozi kuwa makini katika kuendesha chama hususani katika uandaaji na utunzaji wa taarifa, baada ya kugomea taarifa ya ukaguzi wa hesabu za chama kwa madai kuwa taarifa ya Bodi ya chama ina kasoro hivyo haikuwepo Mkutanoni.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa