• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC Telack awataka Wakuu wa Wilaya kukusanya mapato

Posted on: August 6th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amewataka Wakuu wa Wilaya hususani za Kahama na Shinyanga kuhakikisha wanasimamia ukusanyaji wa mapato na kutafuta vyanzo vipya vya mapato katika Wilaya zao.

Mhe. Telack ametoa agizo hilo mapema leo wakati wa hafla fupi ya kumuapisha Mkuu mpya wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Venant Mboneko katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi yake.

Amesema kuwa, kazi kubwa waliyonayo Wakuu wa Wilaya ni kusimamia ukusanyaji wa mapato na kutafuta vyanzo vipya "Tupo zamu kumsaidia Mhe. Rais kuyasimamia yote aliyoyapanga lengo ni kuhakikisha tunatekeleza yote yaliyoainishwa katika Ilani" amesema Mhe. Telack.

Telack amewataka pia Wakuu hao wa Wilaya ambao wameteuliwa hivi karibuni kuhakikisha ujenzi wa miradi mbalimbali unakamilika kwa viwango vinavyotakiwa vikiwemo vituo vya Afya, lakini pia kuimarisha hali ya ulinzi na usalama wa Wilaya za Kahama na Shinyanga na kukataa kurubuniwa kwa rushwa ya aina yoyote.

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa Mhe. Telack ametoa rai kwa viongozi wa Dini kuendelea kuomba dua na sala ili kudumisha amani katika Mkoa wa Shinyanga. 

" Sala na dua ni muhimu sana, watu wanasema Shinyanga imetulia, haitulizwi na Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya pekee, bali ni kwa sala na dua zenu" amesisitiza Mhe. Telack.

Aidha, Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Anamringi Macha akijitambulisha rasmi kwa viongozi na watendaji amesema kipaumbele chake cha kwanza katika Wilaya ya Kahama ni kuhakikisha Kahama inakuwa sehemu salama ya kila mtu kuishi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Nyabaganga Taraba amewakaribisha Wakuu wa Wilaya za Kahama na Shinyanga na kuwahimiza ushirikiano na kumtegemea Mungu katika kutekeleza vema majukumu yao.

Viongozi mbalimbali wakiwemo wa Dini, Vyama vya Siasa na Watendaji pia wakitoa salamu zao katika hafla hiyo, wamewakaribisha Wakuu hao wa Wilaya na kuwaahidi ushirikiano katika kipindi chote watakachokuwa katika Mkoa huu.



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa