• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC Telack apiga marufuku bidhaa za vyakula kuwekwa juani

Posted on: December 4th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amepiga marufuku bidhaa za vyakula kuuzwa zikiwa nje ya maduka hali inayochangia bidhaa hizo kupigwa na jua hivyo kupoteza ubora na kugeuka sumu kwa watumiaji.

Mhe. Telack ametoa marufuku hiyo huku akiwataka Maafisa Afya kusimamia suala hilo katika kikao cha maandalizi ya mpango wa Bajeti ya lishe kwa mwaka 2020 /2021 kilichofanyika Jumatatu ya tarehe 02 Desemba, 2019 Ofisini kwake.

Amesema Maafisa Afya wakisimama katika nafasi zao wataweza kuhakikisha wananchi wanakula vyakula vyenye ubora na kupunguza hatari ya maradhi yanayotokana na sumu za vyakula vilivyopigwa jua.

Aidha, Mhe. Telack amehimiza elimu ya lishe kuanzia utungaji wa mimba hadi miaka mitano kwa watoto itolewe katika kila Kituo cha Afya kabla ya kuwapima akina mama wajawazito, ili wananchi wapate uelewa na kupunguza tatizo la udumavu katika Mkoa.

Amesema kama watoto watalishwa vizuri suala la udumavu litapungua na kwisha kabisa hivyo kupunguzia Serikali bajeti kubwa ya dawa inayoongezeka kila mwaka.

"Serikali inaongeza bajeti ya dawa kila siku kwa sababu watu hawali vizuri wanaugua, tusipoangalia suala hili tutakuwa na Taifa la lenye watu wadumavu ndiyo maana Serikali imelishikia bango" amesema Telack.

Naye Mratibu wa Lishe kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Bw. Mwita Waibe amesema kuwa, nchi inatumia fedha nyingi sana kwenye matibabu na vifaa tiba ikiwemo dawa, vitanda, mashuka na vifaa vya Maabara kwa sababu tu ya ukosefu wa lishe duni.

Afisa Lishe kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Bw. Japhari Magesa akiwasilisha mada ya umuhimu wa lishe amesema kuwekeza katika lishe ni muhimu kwa kuongeza kiwango cha uelewa na ufaulu katika Elimu huku akitoa takwimu kuwa watoto wenye udumavu duniani ni milioni 151 huku watoto wenye udumavu Tanzania ni milioni 3.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa