• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RD MNDEME AITAKA TARURA KUSAFISHA NA KUZIBUA MITARO NA MADARAJA

Posted on: November 20th, 2023

Na. Sinyanga RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina S. Mndeme leo tarehe 20 Novemba, 2023 akiwa ameongozana na wataalamu kutoka Tarura Mkoa na Wilaya ya Shinyanga ametembelea na kukagua miundombinu ya barabara na madaraja kwa ajili ya kuona uimara wake kabla ya mvua kubwa zinazotarajiwa kunyesha kwa mujibu wa Mamlaka ya Utabiri wa Hali ya Hewa Tanzania huku akimuagiza Mhandisi wa Tarura Wilaya ya Shinyanga kuhakikisha wanazibua na kusafisha mitaro pamoja na madaraja kabla ya mvuakuanza.

Mhe. Mndeme ametoa maagizo hayo mara baada ya kukagua madaraja mawili ya Kitangili, ujenzi wa barabara ya Kongo wa kiwango cha lami Mita 145 yenye thamani ya Milioni 88 iliyopo mtaa wa Lumumba, uzibuaji wa daraja la Tambukareli Kata ya Ndembezi hapa Manispaa ya Shinyanga na kuwataka wananchi kuhakikisha wanailinda nankuitunza miundombinu hii ili iwe msaada kwa sasa na baadae.

"Leo tumetembelea na kukagua miundombinu ya barabara na madaraja ambayo inqhudumiwa na Tarura, pamoja nq pongezi kwa kazi wanazozifanya, lakini niwatake Tarura kuhakikisha mnazibua na kusafisha mitaro yote pamoja na madaraja ili iwe tayari kukabiliana na mvua kubwa inayotarajiwa kunyesha kwa mujibu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania," alisema Mhe. Mndeme.

Kwa upande wake Mhandisi Samson Pamphili wa Tarura Wilaya ya Shinyanga alisema kuwa, wamepokea maagizo ya Mhe. Mndeme na kwamba watatekeleza haraka ili kwenda na wakati kwani tahadhari imekwishatolewa juu uwepo wa mvua kubwa.

Eng. Samson aliongeza kusema kuwa, wao Tarura wanaendelea na uzibuaji wa mitaro na usafishaji katika mji wote huku akiwataka wananchi kuacha kufanya shughuli za kibinadamu kandokando ya miundombinu hii inayotekelezwa ili isiharibike na badala yake kila mmoja awe mlinzi wa mwenzie ili iweze kudumu.

"Nitumie nafasi hii kuwaomba wananchi wote kuacha kufanya shughuli za kibinadamu kandokando  ya miundombinu hii ili isiharibike, na badala yake tuitunze zaidi, na pia niwaombe viongozi wa serikali za mitaa wote wasaidie katika utoaji wa elimu hii kwa wananchi wao kupitia mikutano yao na vikao," alisema Eng. Samson.

HABARI PICHA



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa