• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI ITAENDELEA KUSHIRIKIANA NA VYOMBO VYA HABARI ILI KUTEKELEZA TAKWA LA KUHABARISHA UMMA.

Posted on: May 18th, 2023

Na Shinyanga RS.

Serikali imesema inatambua na kuheshimu mchango mkubwa wa vyombo vya habari katika muktadha wa kuhabarisha umma na kuleta maendeleo kwa wananchi.

Hayo yamesemwa leo tarehe 18 Mei, 2023 na Mhe. Johari Samizi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga wakati akiongea na waandishi wa habari pamoja na wadau wa habari alipomuwakilisha Mhe. Christina Mndeme ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga katika Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyoandaliwa na Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club) katila Ukumbi wa Mikutamo uliopo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Pamoja na kuwahakikishia ushirikiano wa Serikali, lakini pia Mhe. Johari amekuwambusha juu ya umuhimu wa kuzingatia maadili ya uandishi wa habari yenye weledi, tija na zenye kuelimisha jamii ili kuiheshimisha taaluma ya habari pamoja Taasisi zao wanazozifanyia kazi.

"Niwahakikishie kuwa, Serikali itaendelea kushirikiana nanyi wakati wote kwakuwa inatambua na kuheshimu mchango wenu kwa umma na Taifa kwa ujumla, lakini pia niwatake mzingatie maadili ya taaluma zenu wakati wote mnapkuwa mnatekeleza majukumu yenu, nasi kwa upande wetu kama Serikali tupo tayari kupokea maoni yenu na hizi changamoto mlizowasilisha tumezichukua", alisema Mhe. Johari

Akitoa salamu kwa niaba ya Shinyanga Press Club Ndg. Greyson Kakuru pamoja na mambo mengine aliainisha baadhi ya changamoto wanazokabiliana nazo katika kazi zao ikiwa ni pamoja na baadhi ya watendaji wa Serikaki kuwa na urasimu wa kuwanyima taarifa za shughuli mbalimbali za maendeleo zinazofanyika, kupewa vitisho pindi wanapofichua miradi ambayo iko chini ya viwango na wanapofuatilia masuala ya kijamii ikiwamo yanayohusu ukatili wa kijinsia ya wanawake na watoto.

Kwa upande wake Meneja Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Mhandisi Fransic Mihayo aliwaambia waandishi wa habari na wadau kuwa, ni vema kwa yeyote anayetaka kufanya kazi ya habari akasomea taaluma hiyo kikamilifu ili aendane na matakwa ya Sheria ya habari ya mwaka 2016, huku akiwataka wale wote wanaoendesha shughuli za kuhabarisha wananchi kupitia Online TV au Blogs kuzisajili na kupata leseni zitakazo waruhusu kufanya kazi hizo bila usumbufu.

Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani hufanyika kila mwaka Mei 3 kwa ajili ya kufanya tathimini ya mchango wa vyomno vya habari ambapo Mkoa wa Shinyanga umeadhimisha tarehe 18 Mei, 2023 kwa kuzingatia ratiba kutoka Umoja wa Klabu za Habari Tanzania  (UTPC) ambao unaagiza kila Klabu kupanga tarehe ya maadhimisho ndani ya mwezi Mei.

Picha ikionesha baadhi ya wanahabari na washiriki wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya Mhe. Johari Samizi wakati wa maadhimisho

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa