Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI ITAENDELEA KUTEKELEZA ILANI YA CCM KWA VITENDO" DC MBONI MHITA

Posted on: February 20th, 2024

Na. Shinyanga RS

MKUU wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita ambaye amemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme amesema kuwa Serikali itaendelea kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) 2020/2025 kwa vitendo na kwa weledi mkubwa ili kuwaletea maendeleo wananchi huku akisisitiza kuwa na ndiyo maelekezo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa CCM Taifa.

Haya yamesemwa leo tarehe 20 Februari, 2024 wakati wa ziara ya Kamati ya Siasa Mkoa wa Shinyanga katika Halmashauri ya Ushetu ambapo jumla ya miradi ya maendeleo mitatu ikiwemo Shule ya Sekondari Dakama, Shule ya Msingi Ukune na Hospitali ya Halmashauri ya Ushetu ambapo kabla ya kukaguliwa mradi wa mwisho Kamati pia ilifanya Mkutano wa hadhara katika kijiji cha cha Ukune ambapo imepokea, kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

"Ndugu Mabala Mlolwa Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Shinyanga, wajumbe wa kamati na wananchi wote, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme napenda kusema kuwa sisi Serikali tatuendelea kutekeleza Ilani ya CCM kwa vitendo, kwa weledi mkubwa sana na tunatekeleza ahadi ya CCM ya kuwaletea maendeleo yenye tija kupitia sekta mbalimbali kama inavyojionesha kwenye miradi hii ya kimkakati", amesema Mhe. Mboni.

Pamoja na pongezi kwa Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Prof. Siza Tumbo na Serikali ya Mkoa kwa ujumla kwa kazi nzuri wanayoifanya kwa wananchi, lakini pia Mwenyekiti wa Kamati Ndg. Mabala Mlolwa ameishauri Serikali kutoa elimu zaidi kwa wananchi ili kuona umuhimu wa kuchangia chakula kwa wanafunzi mashuleni ili waweze kupata chakula mchana au uji asubuhi jambo ambalo litatoa hamasa ya kusoma, kupunguza kabisa utoro na kuimarisha usikivu kwa wanafunzi darasani.

Kamati ya Siasa Mkoa wa Shinyanga inaendelea na ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kuona jinsi gani Ilani ya CCM 2020 / 2025 inavyotekelezwa katika Mkoa ambapo leo ni zamu ya Halmashauri ya Msalala, na kesho tarehe 21 Februari ni zamu ya Manispaa ya Kahama.


HABARI PICHA



Picha hapo juu ni muonekano wa baadhi ya majengo na vifaa tiba katika Hospitali ya Halmashauri ya Ushetu - Kahama.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI MKUU WA TANESCO AMKABIDHI MKUU WA MKOA WA SHINYANGA JIKO LA KISASA LA UMEME

    June 09, 2025
  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa