• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Serikali Mkoani Shinyanga yaendelea kuwakamata wahujumu Uchumi

Posted on: July 1st, 2019

Serikali Mkoani wa Shinyanga imekamata mifuko ya bandia zaidi ya elfu 20 yenye nembo za makampuni ya sukari Nchini inayotumika kubeba sukari isiyokuwa na viwango na kuisambaza kwenye masoko wakati sukari ya viwanda inayozalishwa na viwanda vya ndani ya nchi haitoki kwenye viwanda.

Mifuko hiyo imekamatwa kupitia kikosi kazi maalumu kilichoundwa na Mkoa ili kuendelea na zoezi lililoanza Mwezi Oktoba mwaka jana 2018 lenye lengo la kuwakamata wahujumu uchumi Mkoani hapa. 

Akitoa taarifa ya zoezi hilo mapema leo tarehe 1 Julai, 2019 mbele ya waandishi wa Habari, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amesema kutokana na taarifa za raia wema, watu 14 akiwemo raia mmoja wa kigeni wamekamatwa katika Wilaya za Kahama, Nzega, Igunga na Mkoani Arusha kwa makosa ya uhujumu uchumi ikiwemo kutengeneza, kuuza na kumiliki mifuko na vifungashio bandia.

Mhe. Telack amesema mifuko hiyo ya kampuni tofauti ikiwemo ya Kagera Sugar na Kilombero Sugar, kama ingeingia sokoni ingeweza kupakiwa sukari tani 1000 yenye thamani ya shilingi bilioni 2 na kuwa, viwanda vya ndani visingeweza kuzalisha.

"Sukari hii ingeingia kwenye soko maana yake ni kwamba, hivi viwanda vya ndani visingeweza kuzalisha kwa sababu sukari ambayo haijulikani inatoka wapi ipo sokoni, kitendo hiki ni uhujumu uchumi na kukwamisha juhudi za Serikali za kulinda viwanda vya ndani" amesema Telack.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga  ACP Richard Abwao amesema kuwa, raia wa kigeni ndiye amekamatwa katika Mkoa wa Arusha kwa kosa la uingizaji wa mifuko hiyo inayodhaniwa kutengenezwa katika kiwanda kimoja cha nchi ya jirani na tayari watuhumiwa wote wamefikishwa mahakamani Mkoani Shinyanga na Tabora.

Telack amewataka wananchi watoe taarifa endapo wakiona kuna watu wanafanya biashara za kuuza bidhaa zisizojulikana, Mkoa una kikosi kazi ambacho kipo tayari kwenda Mkoa wowote. 



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa