• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Serikali Mkoani Shinyanga yakamata kadi 267 za "ATM" za Watumishi wa Umma kwenye Taasisi ya kukopesha fedha

Posted on: May 4th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akiwa na Kamati za Usalama za Mkoa na Wilaya ya Shinyanga amekamata jumla ya kadi  za kutolea fedha 267za benki tofauti ambazo ni mali ya Watumishi wa Umma wa Mkoa wa Shinyanga pamoja na kadi za bima za afya, vitambulisho vya kazi na vitambulisho vya kupigia kura katika taasisi ya kukopesha fedha ya Mara Credit Co, Ltd (MCCL) iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga, leo tarehe 04 Mei, 2019.

Taasisi hiyo inayojihusisha na kukopesha fedha kwa watumishi wa Umma na watu binafsi kwa kuchukua kadi zao na namba za siri kwa lengo la kutoa fedha kwenye akaunti zao mshahara unapoingia, imebainika pia kuwakamata watumishi wa umma na kuwafungia kwenye chumba ndani ya Ofisi hiyo pale wanaposhindwa kulipa madeni yao.

Meneja wa taasisi ya hiyo Bw. Cleophace Steven amehojiwa na kukiri kuwa, wanatoa mikopo na kuchukua kadi za watumishi kwa lengo la kutoa fedha kwenye akaunti za wadaiwa wao.

Mhe. Telack akifanya ukaguzi wa Ofisi hiyo, amewaagiza waajiri wote wa taasisi za Umma kusimamia watumishi wao na kuhakikisha kadi zao za kutolea fedha wanazo na kama zipo kwenye taasisi za kukopesha fedha zitakamatwa.

“Naahidi watumishi wa Mkoa huu watafanya kazi bila msongo wa mawazo, nyie mnawatengenezea msongo wanashindwa kufanya kazi kwa amani, nawaambia kwenye Mkoa huu nafasi hiyo haipo! masharti yaliyoanzisha taasisi zenu hayakuwaambia mfanye hivyo” amesema Mhe. Telack.

Amemtaka pia Katibu Tawala Mkoa kuhakikisha anapata orodha ya watumishi wote ambao kadi zao zipo kwenye taasisi za kukopesha fedha na watu binafsi wanaokopesha fedha.

Aidha amemtaka meneja wa Mamlaka ya Mapato Mkoa kuwasilisha taarifa Ofisini kwake inayoonesha mapato yanayopatikana kutokana na biashara hiyo.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa