• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI YAAHIDI KUWAWEZESHA TZS. MILIONI 22 LUMOLUMO WOMEN GROUP

Posted on: May 24th, 2023

Na. Shinyanga RS.

Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita ameahidi kuwasaidia Tzs. Milioni 22 kupitia Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala Kikundi cha Wanawake Lumolumo kilichopo Kijiji cha Namba Moja, Kata ya Segese Halmashauri ya Msalala Mkoa wa Shinyanga.

Ahadi hiyo imetolewa wakati wa ziara ya Mhe. Mboni aliyemuwakilisha Mhe. Christina Mndeme Mkuu wa MKoa wa Shinyanga na wadau mbalimbali wa maendeleo wakiwamo UN- WOMEN, KOICA na TAHA ambapo alitembelea na kukagua shughuli mbalimbali za uzalishaji mali ilkiwamo shamba, ushonaji upishi nk.

“Ombi lenu nimelipokea, na kwa bahati nzuri leo tupo wote hapa na Mkurugenzi wa Msalala, sasa nimuombe rasmi hapa hapa alichukue ombi lenu la Milioni 22 na aende akaliweke kwenye mpango wa mikopo isiyokwa na riba itolewayo na Halmashauri ili mwaka wa fedha ujao muweze kupewa na mfungue hilo duka lenu kama mradi wa kikundi na mfikie malengo yenu kama mlivyokusudia, hili limekwisha chapeni kazi,” alisema Mhe. Mboni.

Awali akisoma taarifa Mwenyekiti wa Kikundi cha Lumolumo alisema kwamba pamoja na mafanikio kiasi waliyoyapata, lakini waliomba wadau kutoka TAHA, UN-WOMEN na Halmashauri kuendelea kuwashika mkono kwa kuwazesha kuongeza mtaji ili waweze kufungua duka litakalokuwa na thamani ya Milioni 27 ambapo wao wanayo Milioni 5 zilizopo Benki.

Kufunguliwa kwa duka hilo kutapelekea kusogeza huduma karibu zaidi na wakulima wa Halmashauri ya Msalala na Kahama ambapo wataweza kupata mbegu na pembejeo na kwamba wanatarajia kuwa Wakala mkubwa na muhimu Zaidi kwa Mkoa wa Shinyanga.

Kikundi cha Lumolumo kilianzishwa rasmi Septemba, 2019 kikiwa na wananchama 12 wote wanawake, ambapo sehemu ya mafanikio ni pamoja na kuchimba kisima cha maji chenye urefu wa futi 100 chenye thamani ya Milioni 32, kutengeneza miundombinu ya shamba yenye thamani ya Milioni 32 yote hayo yakisimamiwa na Halmashauri pamoja na TAHA.

Picha ikionesha sehemu ya wanachama wa Lumolumo Women Group

Moja kati ya shamba la Lumolumo Women Group likiwa kwenye maandalizi ya kupanda mbegu

Sehemu ya shamba la mahindi linalomilikiwa na kikundi cha Lumolumo

Picha ikionesha sehemu ya miundombinu (NISHATI YA MWANGA WA JUA) inayowezesha wanakikundi wa Lumolumo kufanya shughuli zao za uzalishaji 


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa