• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI YAITAKA KAMPUNI YA CHICO KUTEKELEZA MRADI NDANI YA MUDA ULIOPANGWA

Posted on: May 30th, 2023

Na. Shinyanga RS.

Serikali imeitaka Kampuni ya China Hennan International Corperation Group Co. Ltd (CHICO) iliyopewa kandarasi ya kufanya maboresho makubwa katika Uwanja wa Ndege wa Mkoa wa Shinyanga inatekeleza kazi hiyo na kukabidhi ndani ya muda uliopangwa.

Hayo yamesemwa na mgeni rasmi Mhe. Johari Samizi Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga aliyemuwakilisha Mhe. Christina Mndeme ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga katika Hafla ya Utambulisho wa Mradi wa Maboresho ya uwanja huo yaliyofanyika katika eneo la Ofisi ya Uwanja wa Ndege iliyopo Kata ya Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga Mkoa wa Shinyanga na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwamo Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Pro. Siza D. Tumbo, Kamati za Ulinzi, viongozi wa Dini na wadau mbalimbali wa Usafiri wa Anga.

“Nitoe rai kwa (CHICO) ambaye ndiye mkandarasi wa maboresho haya makubwa ya uwanja wetu wa ndege kuhakikisha anafanya kazi hii kwa weledi, uaminifu, viwango na uzalendo mkubwa huku akizingatia muda uliowekwa na aweze kukabidhi kwa wakati ili wananchi wa Mkoa wa Shinyanga waanze kunufaika na kufurahia huduma hii ambayo kwa sasa wanalazimika kuifuata Mkoa wa Mwanza ambapo hulazimika kutumia Kilomita 164 kutokea hapa Shinyanga,” alisema Mhe. Johari.

Awali akisoma taarifa ya maboresho hayo Meneja Mradi Viwanja vya Ndege – TANROAD Makao Makuu Mhandisi Neema Joseph alisema kuwa mkandarasi atatumia miezi 18 (Aprili, 2023 hadi Oktoba, 2024) na kwamba katika kazi hiyo itakayogharimu zaidi ya Bilioni 49 za Kitanzania fedha zitokanazo na Ufadhili wa Benki ya Uwekezaji kutoka Ulaya.

Kwa upande wake Meneja TANROAD Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Mibara Ndirimbi alisema kuwa, pamoja na kazi nyingine lakini mkandarasi atafanya maboresho na kutengeneza barabara ya kuruka na kutua ndege kwa kiwango cha lami, barabara ya kiungio na maegesho ya ngede kwa kiwango cha lami, jengo jipya la kupumzikia abiria lenye uwezo wa kuchukua watu 150 hadi 250 kwa wakati mmoja, barabara ya kuingia uwanjani pamoja na jengo la Huduma za Hali ya Hewa huku akitumia fulsa hiyo kuwataka wananchi wa Mkoa wa Shinyanga kuulinda mradi huo na kuepuka vitendo vyovyote vya hujuma.

“Pamoja na shukurani kwa Serikali yetu, lakini niwaombe pia wananchi wa Mkoa wa Shinyanga kwa umoja wetu tushirikiane katika kuulinda mradi huu bora kabisa kwa maslahi yatu na Taifa ili kusiwepo na vitendo vyovyote vya hujuma na mwisho tuje kunufaika na kufurahia uwepo wa Uwanja huu hapa Shinyanga,” alisema Mhandisi Ndirimbi 

Kukamilika kwa mradi huu unaoboreshwa kuwa na urefu wa kilomita 2 na upana wa mita 30 za upana wa njia ya kurukia na kutua kwa ndege kunatajwa kwenda kuwaondelea adha kubwa wanaoyoipata wananchi wa Mkoa wa Shinyanga pamoja na maeneo jirani sambamba na kuongeza mzunguuko wa fedha jambo ambalo litainua uchumi wa mtu mmoja mmoja wa Mkoa na kuongeza pato kwa Taifa kwa ujumla wake.

Picha ikionesha wajumbe wakikagua moja kati ya barabara zitakazotengenezwa na mkandarasi CHICO

Picha ikimuonesha Meneja TANROAD Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Mibara Ndirimbi akielezea jambo wakati wa hafla ya utambulisho wa mradi wa uboreshaji wa upanuzi wa uwanja wa ndege


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa