• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

SHINYANGA YAENDELEA KUPAMBANA NA MAAMBUKIZI YA VVU KWA VIJANA BALEHE KUPITIA USIMAMIZI SHIRIKISHI

Posted on: October 17th, 2025

Na Johnson James- Shinyanga

Serikali ya Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Wizara ya Afya, UNICEF na wadau wengine wa maendeleo, imefanya kikao kazi muhimu kwa ajili ya kujadili mikakati ya kuboresha huduma za afya kwa vijana balehe, hasa katika mapambano dhidi ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU).

Akifungua kikao hicho, Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga David Lyamong ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimaliwatu amesema kuwa lengo kuu ni kuhakikisha kundi la vijana balehe linafikiwa na huduma bora za afya zikiwemo za lishe, afya ya akili na afya ya uzazi, ili kulinda afya na mustakabali wa kundi hilo muhimu katika maendeleo ya taifa.

Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, Mkoa wa Shinyanga una vijana balehe wapatao 449,038 wenye umri wa miaka 15 hadi 24. Hata hivyo, hali ya maambukizi ya VVU kwa kundi hili ni ya juu kwa asilimia 6.2, ukilinganisha na wastani wa kitaifa wa asilimia 3.7. Hali hii imepelekea mkoa kuchukua hatua madhubuti kupitia ushirikiano wa karibu na wadau mbalimbali.

“Tumeendelea kusimamia afua mbalimbali za VVU na UKIMWI katika Halmashauri zote sita za mkoa wetu kwa lengo la kuimarisha afya za vijana balehe. Vijana hawa wanakumbana na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na lishe duni, afya ya akili na afya ya uzazi. Tunajitahidi kuhakikisha wanapata huduma bora, japo ufinyu wa rasilimali bado ni changamoto,” alisema mtoa hotuba.

Katika hatua za awali za utekelezaji, zoezi la usimamizi shirikishi limefanyika kati ya tarehe 15 hadi 16 Oktoba 2025 katika Manispaa za Kahama na Shinyanga pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Msalala. Kazi hii imewezesha kubainisha maeneo yenye mafanikio pamoja na changamoto zinazohitaji suluhisho la haraka.

Kikao kazi hiki kinatarajiwa kuibua maazimio ya pamoja yatakayosaidia kuongeza ufanisi wa utoaji huduma kwa vijana, pamoja na kuweka mikakati endelevu ya kupunguza maambukizi mapya ya VVU miongoni mwa vijana.

Mkoa wa Shinyanga umeahidi kuendelea kushirikiana na TACAIDS na wadau wote wa maendeleo kuhakikisha kuwa juhudi za kukabiliana na VVU/UKIMWI kwa vijana zinaimarika, na hatimaye kufikia kizazi kisicho na maambukizi mapya ya VVU.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa