• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

SHINYANGA YANG'ARA MICHEZO YA UMITASHUMTA 2023 TABORA

Posted on: June 3rd, 2023

Na. RS SHY - Tabora

MKOA wa Shinyangaa umeibuka kidedea katika michezo ya ufunguzi wa Mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa wanafunzi wa Shule za Mshingi Tanzania (UMITASHUMTA) ambayo yamefunguliwa Mjini Tabora ambapo yanafanyika kitaifa na kuhusisha Mikoa yote ya Tanzania.

Mkoa wa Shinyanga umeibuka kinara katika michezo ya mpira wa miguu (kundi maalumu) ambapo imeshinda 9 - 0 dhidi ya Katavi, mpira wa miguu Shinyanga imeshinda 1- 0 dhidi ya Songwe, mpira wa mikonno wasichana Shinyanga imeshinda 21 - 10 dhidi ya Rukwa pamoja goalball ambapo Shinyanga imeshinda 24 - 8 dhidi ya Kagera.

Mashindano haya amabayo yanahusisha michezo mbalimbali yamefunguliwa leo Juni 03, 2023 na Naibu Katibu mkuu anayeshughulikia Elimu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR – TAMISEMI), Dkt. Charles Msonde.

Katika hotuba yake Dr. Charles Msonde amesisitiza juu ya uadilifu wakati wa michezo ya UMITASHUMTA mwaka huu wa 2023, ikiwepo udhibiti wa wanamichezo wasioruhusiwa (MAMLUKI) ili kuipa heshima sekta ya michezo mashuleni.

Akitoa maoni yake kuhusu michezo ya mwaka huu, Afisa Utamaduni Mwandamizi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Janeth Elias amewapongeza waandaji kwa maandalizi mazuri.

“Serikli kupitia waandaaji wamejitahidi sana kuboresha kila eneo, hii inaonyesha namna ambavyo vijana watayafurahia mashindano ya mwaka huu kwa kipindi chote watakachokuwa hapa Tabora, pongezi hizi ziende kwa Rais wetu Dk.Samia Suluhu Hassan” amesisitiza Bi. Janeth Elias.

Mashindano ya UMITASHUMTA & UMISETA mwaka 2023, yanaandaliwa na kusimamiwa na Ofisi ya Rais – TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Mkoa wa Tabora ni mwenyeji wa mashindano haya kwa mwaka wa pili mfulululizo, ikiwa mwaka jana 2022 pia mashindano yaliandaliwa na Mkoa wa Tabora.

Picha ikionesha baadhi ya wachezaji wa timu ya mpira wa miguu kutoka Mkoa wa Shinyanga wakiwa uwanjani

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa