• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

TUME YA TAIFA YA MIPANGO YA MATUMIZI YA ARDHI YAKUTANA NA MKUU WA MKOA WA SHINYANGA, YAAHIDI KUTOA HATI ZAIDI YA 1,000 KWA WANANCHI WA USHETU.

Posted on: September 15th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, leo Septemba 15, 2025, amekutana na ujumbe kutoka Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi ofisini kwake, kwa lengo la kujadiliana kuhusu hatua za kuimarisha upatikanaji wa hati miliki na matumizi bora ya ardhi mkoani humo, hususan katika Wilaya ya Ushetu.

Katika kikao hicho, Naibu Kamishna wa Tume hiyo kwa Mkoa wa Shinyanga, Bw. Leo Komba, ameahidi kuwa zaidi ya hati 1,000 zitatolewa kwa wananchi wa Ushetu kama sehemu ya juhudi za Serikali kuimarisha usalama wa milki za ardhi na kupunguza migogoro.

Mhe. Mhita ameipongeza Tume hiyo kwa hatua wanazochukua katika kuhakikisha wananchi wananufaika na ardhi yao kwa mujibu wa sheria. Amesema changamoto ya umiliki holela wa ardhi ni moja ya vikwazo vya maendeleo, hivyo upatikanaji wa hati utasaidia sana kuleta suluhu ya kudumu.

"Kupitia zoezi hili, tunatarajia kuona mwamko mkubwa wa wananchi kushiriki na kupata haki yao halali ya kumiliki ardhi. Hii pia itawawezesha kuitumia ardhi yao kama dhamana ya mikopo na fursa nyingine za maendeleo," amesema Mhe. Mhita.

Kwa upande wake, Bw. Komba amesema kazi hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi ulioidhinishwa na Serikali, unaolenga kuimarisha matumizi sahihi ya ardhi, kukuza kilimo, biashara na utulivu wa kijamii.


Zoezi hilo la utoaji wa hati linatarajiwa kuanza mara moja katika vijiji mbalimbali vya Ushetu, ambapo wananchi watahamasishwa kushiriki kikamilifu ili kuhakikisha kila mmoja anapata hati yake kihalali na kisheria.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa