• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

TUMIENI MUDA HUU ULIOBAKIA KUJISAJILI NA KUSHIRIKI SHYCOM ALUMNI MARATHONI - RC MACHA

Posted on: September 14th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ametoa wito kwa wananchi wote kujitokeza, kujisajili ili waweze kushiriki vema katika tukio muhimu la mbio za Shycom Alumni Marathoni litakalofanyika tarehe 21 Septemba, 2024 huku lengo kuu likitajwa kuwa ni kuchangia fedha zitakazoboresha miundombinu ya Chuo cha Shycom.

Macha ameyasema haya leo tarehe 14 Septemba, 2024 ofisini kwake alipokuwa akizungumza na wanahabari kuhusu umuhimu wa tukio hili ambapo pamoja na mambo mengine lakini pia amesema mbio hizi zitawezesha kuimarisha uhusiano, kuboresha afya, kutambua na kujenga vipaji, kuchangia damu na kwamba takribani washiriki 1000 wanatajiwa katika tukio hili.

"Naomba kutoa wito kwa wananchi wote kujitokeza, kujiandikisha na kushiriki kikamilifu katika mbio hizi za hisani zilizopewa jina Shycom Alumni Marathoni ili tuweze kutimiza lengo la kuchangia fedha kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu, kuimarisha umoja, uhusiano wetu, kuboresha afya zetu, kubainisha na kujenga vipaji kwa vijana wetu na kuchangia damu itakayowasaidia wagonjwa katika vituo vyetu vya afya," amesema Macha.

Aidha, Serikali ya Mkoa wa Shinyanga imewahakikishia usalama wakati wote wanamichezo wote watakaofika hapa mkoani Shinyanga na kushiriki katika Shycom Alumni Marathoni huku wafanyabiashara kutumia vema fursa ya uwepo wa mbio hizi kwani watu 1000 siyo wachache.

Shycom Alumni Marathoni ni mbio za hisani ambazo zimeandaliwa kwa maalum kwa waliosoma au kupita Shycom tangu kuanzishwa kwake wakiwemo waliokuwa Wadhibiti na Wakaguzi Wakuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kama vile Charles Kichere na ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Elimu Mhe. Adolf Mkenda (MB) sanjari na mwenyeji wake ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Macha.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa