• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

TUTAENDELEA KUWASHUGHULIKIA WATUMISHI WASIOKUWA NA MAADILI

Posted on: May 20th, 2024

Na. Paul Kasembo, Msalala.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amesema kuwa Serikali itaendelea kushughulika na watumishi wachache ambao wasiokuwa waadilifu, wazembe na wenye nia ya kuharibu taswira nzima ya utendaji kazi wa Serikali.

RC Macha ameyasema haya leo tarehe 20 Mei, 2024 alikuwa akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kikao ambacho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo ofisi ya Mkurugenzi wa Msalala huku akiwataka watumishi kuwa waadilifu, kutumia lugha nzuri katika kuwahudumia wananchi na kuchapa kazi zaidi ili kumsaidia Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye maono yake ni kuhakikisha kuwa wananchi wanapata maisha bora.

"Tutaendelea kuwashughulikia watumishi wachache wasiokuwa waadilifu na wazembe wenye nia ya kuichafua taswira ya Serikali, kwakuwa siyo kweli kwamba watumishi wote wanazo tabia mbaya kwa hili hapana hatuvumilia mtu", amesema Mhe. Macha.

Akiwasilisha taarifa ya utekeleza wa shughuli za maendeleo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala Ndg. Khamis Katimba pamoja na kumshukuru sana Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuipatia Msalala fedha za maendeleo na na kuwahudumia wananchi.

Aidha Katimba amesema kuwa, Msalala imekuwa ni moja ya Halmashauri iliyopata Hati Safi ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2022/2023, inaendelea kuimarisha na kuboresha utawala bora huku alisema kuwa Halmashauri imeishavuka lengo la makusanyo kwa mwaka wa fedha 2023/2024 huku ikiwa ni mwezi mmoja kabla ya ukomo wa kukusanya kwa mujibu wa Serikali.

RC Macha anaendelea na ziara yake katika Mkoa wa Shinyanga ambapo leo anaiangazia Halmashauri ya Wilaya ya Msalala katika sekta ya afya, utawala na baadae atazungumza na wananchi katika mkutano wa wananchi ambapo atajitambulisha, kupokea, kusikiliza na kutatua kero zao kweye viwanja vya Bugalama.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa