• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

TUWEKE MIKAKATI MADHUBUTI KUKOMESHA MMOMONYOKO WA MAADILI –RC MHITA

Posted on: September 24th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita @mboni_mhita ametoa wito kwa viongozi wa dini, viongozi wa kimila na jamii kwa ujumla kuweka mikakati madhubuti ya kukomesha mmomonyoko wa maadili, hasa miongoni mwa watoto na vijana.

Akizungumza katika kikao kilichoratibiwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kupitia Idara ya afya ustawi wa jamii na lishe kwa kushirikiana na shirika la ICS kilichofanyika leo Septemba 24, 2025 kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mhe. Mhita amesema mmomonyoko wa maadili umechukua kasi kubwa, huku athari zake zikijidhihirisha kwa familia kuvunjika, ongezeko la utoro mashuleni, watoto wa mitaani, na vitendo vya uhalifu.

“Leo hii tunaona familia zikivunjika, watoto wakitoroka mashuleni, wengine wakikimbilia mitaani na kujiingiza kwenye vitendo vya uhalifu. Haya yote ni matokeo ya mmomonyoko wa maadili ambao mizizi yake ni kulegalega kwa malezi katika ngazi ya familia,” alisema

Akitaja sababu kuu zinazopelekea hali hiyo, alieleza kuwa ni pamoja na Wazazi na walezi kushindwa kutimiza wajibu wao, Jamii kujitoa kwenye jukumu la pamoja la malezi, Kukosekana kwa hofu ya Mungu na kuiga mitindo ya maisha ya kigeni isiyoendana na maadili ya Kitanzania.

Aidha, Mhe. Mhita alisisitiza umuhimu wa kutekeleza kwa vitendo Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto, akisema ni njia bora ya kuhakikisha watoto wenye umri wa miaka 0 hadi 8 wanalelewa katika mazingira yenye maadili, usalama na mwongozo wa kimaadili.


“Kama tutafanikiwa kuwalea watoto wetu vizuri kuanzia sasa, tutakuwa na vijana wenye maadili, wanaoheshimu wakubwa, wanaojitambua na wanaowajibika kwa jamii. Hili linawezekana iwapo kila mmoja wetu atachukua jukumu lake kwa uzito,” aliongeza.

Kikao hicho, kiliwashirikisha kamati ya maridhiano na amani mkoa, viongozi wa dini mbalimbali,viongozi toka makundi maalumu kama smaujata. Umoja wa wanaume, Baraza la Wazee Mkoa, vyama vya watu wenye ulemavu, Ofisi ya Magereza Mkoa, wataalumu toka ngazi ya Mkoa na Mdau kinara wa malezi ICS.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA ARIDHISHWA NA UTOAJI HUDUMA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SHINYANGA.

    September 28, 2025
  • WATENDAJI AMCOS WATAKIWA KUWA WABUNIFU ILI KUONGEZA UZALISHAJI NA THAMANI YA MAZAO YA KIBIASHARA.

    September 27, 2025
  • RC MHITA AITEMBELEA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA, ATOA WITO WA KUWEKEZA KATIKA MAADILI NA ELIMU BORA KWA MTOTO WA KIKE.

    September 27, 2025
  • HALMASHAURI SHINYANGA ZATAKIWA KUTENGA BAJETI KUENDELEZA UTOAJI WA HUDUMA ZA MADAWATI YA USTAWI WA JAMII KATIKA STENDI ZA MABASI

    September 27, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AAGIZA MKANDARASI KUKATWA MILIONI 2 KILA SIKU KWA KUCHELEWESHA BARABARA KAHAMA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa