• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

UWANJA WA NDEGE SHINYANGA: NGUZO MPYA YA MAENDELEO NA FURSA ZA KIUCHUMI

Posted on: October 16th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita, amesema kukamilika kwa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga (Ibadakuli) kutakuwa hatua kubwa ya mageuzi katika sekta za uchumi, biashara, utalii na usafiri wa anga ndani ya mkoa na kwa taifa kwa ujumla.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ziara ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa Uwanja huo, Mhe. Mhita alisema:

“Uwekezaji huu mkubwa unaotarajiwa kukamilika hivi karibuni, utafungua milango kwa wafanyabiashara, wakulima na wawekezaji. Tumeuweka uwanja huu kwenye mpango wa kimkakati wa maendeleo ya mkoa ili kuunganisha fursa zilizopo na masoko mapya, ndani na nje ya nchi."

Alisisitiza kuwa Serikali ya Mkoa itaendelea kuimarisha mazingira rafiki kwa uwekezaji, hasa kwa kuzingatia uwepo wa Kongani ya Kitaifa ya Biashara ya Buzwagi, ambayo inalenga kuchochea ukuaji wa uchumi wa ndani.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Kiwanja cha Ndege Shinyanga, Lugano Mwinuka, alieleza kuwa mradi umefikia asilimia 90 ya utekelezaji, na kazi kubwa zinazoendelea ni maboresho ya miundombinu ya kiufundi na kiusalama.

“Tunafanya ukarabati wa njia ya kurukia na kutua ndege (runway), maegesho ya ndege, jengo la abiria, mitaro ya maji, taa za usiku, uzio wa usalama na kituo cha hali ya hewa,” alisema.

Aliongeza kuwa kukamilika kwa uwanja huo kutawezesha ndege aina ya Bombardier Q400 yenye uwezo wa kubeba abiria 74 kutua kwa urahisi. Hii ni hatua itakayopandisha hadhi ya kiwanja kutoka daraja la kwanza hadi la tano katika viwango vya zimamoto na usalama wa anga.

Kaimu Meneja wa TANROADS Mkoa wa Shinyanga, Mhandisi Chiando Mwinuka, alithibitisha kuwa barabara kuu zote zinazounganisha uwanja huo na mikoa jirani kama Tabora na Mwanza tayari zimekamilika.

“Tumejenga barabara ya kisasa inayoingia moja kwa moja uwanjani. Lengo ni kurahisisha usafirishaji wa abiria na mizigo, na kuongeza ufanisi wa huduma za anga katika mkoa wetu,” alisema.

Kwa upande wa wananchi, matumaini ni makubwa. Bi. Esther Maziku, mkazi wa Ngokolo, alisema:

“Zamani tulikuwa tukisafiri hadi Mwanza ili tupate ndege tena kwa kutumia muda mrefu lakini Sasa Uwanja tunao wenyewe, tunamshukuru Rais Samia kwa kutenga fedha na kutuletea Uwanja wa Ndege na sasa  tunaona kama tumeunganishwa na dunia. Hii ni fursa kwa wanawake wajasiriamali kama mimi.”

Mradi wa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga unatazamwa kama kichocheo kikubwa cha maendeleo ya kiuchumi, hasa kwa kuzingatia utajiri wa rasilimali zilizopo mkoani hapa  kuanzia ardhi yenye rutuba, madini, hadi vivutio vya utalii na uwekezaji.

Mradi huo unakadiriwa kugharimu TSh bilioni 52 (pamoja na VAT), ambapo 80% ya fedha zimetolewa na Benki ya Uwekezaji ya Umoja wa Ulaya (European Investment Bank) na 20% inagharamiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania


Kwa kukamilika kwake, uwanja huu utaifanya Shinyanga kuwa kitovu kipya cha biashara na utalii katika Kanda ya Kaskazini Magharibi ya Tanzania, huku ukifungua milango kwa mashirika ya ndege ya ndani na ya kimataifa.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa