• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

VIONGOZI WA DINI SHINYANGA WAHAMASISHA AMANI NA USHIRIKI WA UCHAGUZI OKTOBA 29

Posted on: October 18th, 2025

Na Johnson James, Shinyanga

Viongozi wa dini mkoani Shinyanga wametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025, wakisisitiza kuwa ni haki ya kikatiba na hatua muhimu ya kuchagua viongozi bora watakaowaletea maendeleo ya kweli kuanzia ngazi ya jamii.

Wakizungumza leo Octoba 18, 2025 mkoani Shinyanga kwa pamoja katika tamko lao kwa umma, viongozi hao wakiongozwa na Askofu Dkt Emmanuel Makala wameazimia kuunga mkono jitihada za serikali katika kuhamasisha wananchi kushiriki uchaguzi huo kwa amani na utulivu, huku wakikumbusha kuwa kila Mtanzania ana wajibu wa kulinda amani ya nchi.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, amewatoa hofu wananchi akiwahakikishia kuwa siku ya uchaguzi itakuwa salama na yenye utulivu, huku vyombo vya ulinzi na usalama vikiwa tayari kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani.

"Tunawahakikishia wananchi usalama wao. Waende kupiga kura bila hofu. Serikali imejipanga kuhakikisha kila mmoja anatekeleza haki yake kwa uhuru,” alisema Mhita.

"Amani ni tunu ya taifa letu. Bila amani hakuna maendeleo. Tunawasihi wananchi kujitokeza kupiga kura kwa utulivu, wakitambua kuwa wanatimiza wajibu wao kwa taifa" walisema viongozi hao kwa umoja wao.

Aidha, aliyewahi kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu ameendelea kuwasihi viongozi wa dini, machifu, na wazee kuendelea kuliombea taifa, hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi, akisisitiza kuwa maombi ni silaha ya kuimarisha mshikamano wa kitaifa.

Tamko hilo ni sehemu ya juhudi za pamoja za kuhakikisha uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani unafanyika katika hali ya utulivu, mshikamano na kwa kuzingatia misingi ya demokrasia.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa