• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WAAJIRI SEKTA BINAFSI RUHUSUNI WATUMISHI WENU KUJIUNGA NA CHAMA CHA WAFANYAKAZI - RC MACHA

Posted on: May 1st, 2024

Na. Paul Kasembo, Kakola - Msalala.

MKUU aa Mkoa aa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ametaka waajiri hasa wa Sekta binafsi kuwaruhusu waajiriwa wao ili waweze kujiunga na Chama cha Wafanyakazi chochote ili waweze kunufaika na kuzisaidia sekta zenu kwakuwa ni wajibu na haki kwa pande zote mbili.

Maelekezo haya yametolewa na RC Macha wakati akihutubia wafanyakazi wa Mkoa wa Shinyanga katika kilele cha Siku ya Wafanyakazi Duniani (MEI MOSI) ambayo kwa Mkoa wa Shinyanga sherehe zilifanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Kakola iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Msalala ambapo pamoja na mambo mengine RC Macha aliwaeleza watumishi kuwa suala la Kikokotoo limekwishapokelewa na Serikali na litafanyiwa kazi ukizingatia kuwa limesemewa na Mamlaka mbalimbali.

"Pamoja na kuwapongeza kwa maadhimisho haya leo, nchukue nafasi kuwaelekeza waajiri wote wa Sekta binafsi kuwaruhu watumishi wao kuchagua Chama cha Wafanyakazi chochote na kujiunga kwakuwa ni haki yao nanyi ni wajibu wenu kutekeleza hili," amesema RC Macha.RC

Aidha, RC Macha amewaahidi wafanyakazi wa Mkoa wa Shinyanga kuwa yale yote yaliyosemwa na viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi Mkoa ameyachukua na kwa yale yaliyo ndani ya uwezo wake atayatekeleza haraka na kwa ufanisi zaidi, na kwa yale yaliyo juu ya mamlaka yake ameahidi kuyafikisha tena kwa maandishi bila kupunguza neno lolote.

Kuhusu suala la Kikokotoo, amesema kuwa ni jambo ambalo kwa hivi karibuni limesemwa na mamlaka mbalimbali na hivyo anayoimani kubwa na Serikali kuwa litafanyiwa kazi na pande zote zitakuwa sawa kabisa kwakuwa Serikali hii ni sikivu sana.

Kwa upande wake Mratibu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Mkoa wa Shinyanga alisema kuwa suala la Kikokotoo limekuwa likidhoofisha watumishi sana na hivyo akaiomba Serikali kulifanyia kazi huku akisistiza juu ya vifurushi vyenye maslahi zaidi ka wafanyakazi ili kuongeza ari ya watumishi kufanya kazi zaidi.

Mwaka 1886, vyama vya wafanyakazi vya Marekani vilianzisha mgomo wa watu wengi kudai kufanya kazi saa nane kwa siku , kwa kuzingatia wazo la mwanamageuzi wa kijamii wa Uingereza Robert Owen.


HABARI PICHA

Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita wakati wa sherehe ya Siku ya Wafanyakazi Duniani MEI MOSI - KALOLA, MSALALA.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa