• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Waajiri watoe mafunzo elekezi kwa Waajiriwa wapya

Posted on: August 18th, 2017

Mhadhiri wa Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo 

Dkt. Henry Jonathan akitoa ufafanuzi wa Kiongozi 

cha Mafunzo elekezi ya awali kwa watumishi wapya 

wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za 

Mitaa kwa Wakuu wa Sehemu na Vitengo katika 

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga tarehe 16/08/2017.


Waajiri nchini wametakiwa kutoa mafunzo elekezi kwa waajiriwa wapya katika Sekta za Umma ili kuwapa watumishi hao taarifa sahihi kuhusu haki na wajibu wao wakiwa kazini.

Akitoa ufafanuzi wa kijitabu cha mwongozo wa utaratibu wa mafunzo elekezi ya awali kwa watumishi wapya wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa katika kikao cha pamoja na Wakuu wa Sehemu na Vitengo wa Sekretarieti ya Mkoa wa Shinyanga, mapema wiki hii, mmoja wa washiriki katika kuandaa mwongozo huo, Dkt. Henry Jonathan amesema changamoto nyingi wanazokumbana nazo waajiriwa wapya zinatokana na kukosa taarifa sahihi hivyo kupelekea kukata tamaa na kupoteza morali ya kazi.

Dkt. Henry ambaye ni Mhadhiri wa Chuo cha Serikali za Mitaa – Hombolo Dodoma amesema kuwa, baadhi ya waajiri hawatoi mafunzo kwa waajiriwa wapya kutokana na kutojua umuhimu wa mafunzo hayo pamoja na uhaba wa fedha.

Amesema wakati mwingine mafunzo hayatolewi kwa wakati hivyo kupelekea watumishi hao kufanya vitu ambavyo si sahihi.

Kijitabu hicho ambacho kilishazinduliwa na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. George Simbachawene kinaeleza utaratibu mzima wa namna ya kuwapokea watumishi wapya katika ajira na kuwapa mafunzo elekezi ili kuendana na Sera, Sheria na taratibu za kiutumishi kuanzia ngazi ya Wizara hadi vijiji.

Kijitabu hicho kilichotengenezwa kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI pamoja na Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta ya Umma (PS3) kitasambazwa katika Mikoa yote nchini ili kiwasaidie waajiri kutoa mafunzo elekezi kwa watumishi wapya katika ajira.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa