• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Waandikishaji wa CHF kutambulishwa kwenye nyumba za Ibada

Posted on: April 21st, 2017

Serikali Mkoani Shinyanga kwa kushirikiana na Viongozi wa dini wameazimia kwa pamoja kuwatambulisha waandikishaji wa wanachama wa mfuko wa Afya wa Bima ya Wananchi yaani CHF kwenye nyumba za Ibada ili kupanua wigo wa uandikishaji wa mfuko huo.

Azimio hilo limefikiwa katika kikao cha pamoja kati ya Mkoa na viongozi hao wa dini kilichofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kwa lengo la kuwahamasisha viongozi wa dini kuhusu mfuko huo ili wasaidie kuwahamasisha wananchi ambao wengi ni waumini wa misikitini na makanisa.

Akifungua kikao hicho, Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Bw. Albert Msovela amesema ana imani kubwa na viongozi wa dini katika kuhamasisha wananchi kujiunga na mfuko wa bima ya Afya kwa sababu viongozi wa dini wamekuwa msaada kwa Serikali katika masuala mbalimbali ya kijamii kwa kuwaelewesha wananchi.

“Ni imani yangu kuwa, kila mwananchi ana namna yake ya kuweza kuabudu, viongozi wa dini wana nafasi kubwa ya kuwafikia wananchi pamoja na kuwa Serikali inafanya pia”. Amesema Msovela.

Msovela amewaeleza viongozi hao wa dini kuwa CHF iliyoboreshwa inafanya kazi katika Mikoa mitatu kwa sasa ambapo Shinyanga ni mojawapo ya Mikoa hiyo, hivyo amesema ni bahati kubwa kwa wananchi wa Mkoa kutumia nafasi hii ili kupata matibabu kwa unafuu kwani kwa shilingi elfu kumi tu kwa mwaka, kaya yenye watu 6 watapata matibabu.

Awali, Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Rashid Mfaume akimkaribisha Katibu Tawala Mkoa kufungua kikao hicho amesema, lengo la kikao ni kuwaomba Viongozi wa dini kusaidia kuwahamasisha waumini kujiunga na mfuko wa bima ya jamii iliyoboreshwa, kuhakikisha kuwa, jamii tunayoisimamia inapata huduma. “Jamii yetu wananchi wengi wana kipato kidogo, Serikali imeona kuwa kuna umuhimu mkubwa wa wananchi kupata huduma kwa gharama wanayoimudu”.

Dkt. Mfaume amesema, kutokana na kasi ya uandikishaji kuwa ndogo, Mkoa umewashirikisha viongozi wa dini ambao wataongeza kasi ya uhamasishaji na kusaidia waumini kuona namna ya kuwasaidia wananchi wasio na uwezo kuweza kupata huduma za afya kupitia CHF, hivyo ni vema waandikishaji hawa wafahamike na kuweza kuandikisha wanachama wengi zaidi.

Katika kikao hicho, Mkoa na viongozi hao wa dini wamekubalian masuala mbalimbali ikiwemo kufanya utaratibu wa kupata waandikishaji watakaoandikisha katika nyumba za Ibada, waratibu wa CHF wa Wilaya wafanye utambuzi wa viongozi wa dini katika maeneo yao ili wakae pamoja kupanga mkakati wa uhamasishaji.

  • Aidha, kufanya uhamasishaji kwenye nyumba za Ibada na kuona namna ya kuwasaidia wasio na uwezo na iwe ni ajenda ya kudumu na kuwepo na mahusiano ya karibu kati ya Wataalamu na viongozi wa dini ili kuweza kuelezea kwa mapana suala hili na fursa zinapojitokeza za kwenda pamoja kuhamasisha.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUOMBA NAFASI YA UJUMBE WA BODI YA HOSPITALI YA MKOA January 03, 2020
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha nne 2019 January 09, 2020
  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa Kidato cha pili 2019 January 09, 2020
  • Mwenge wa Uhuru kuwasili Mkoani Shinyanga May 07, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU 100

    June 27, 2021
  • SIKU MIA 100 ZA RAIS SAMIA

    June 27, 2021
  • DKT. SENGATI AHAIDI KUPAMBANA NA CHANGAMOTO YA UMASIKINI SHINYANGA

    June 05, 2021
  • Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga aapishwa

    June 02, 2021
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa