• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WADAU WA MAJI WILAYANI KISHAPU WAAZIMIA KULIPA MADENI YOTE YA RUWASA

Posted on: August 24th, 2024

Na. Paul Kasembo, KISHAPU.

WADAU wa Mkutano Mkuu wa mwaka wa Wadau wa Maji wilayani Kishapu ulioandaliwa na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Kishapu ambao Mwenyekiti wake ni Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude wameazimia kwa pamoja kulipa madeni yote wanayodaiwa na RUWASA ndani ya siku 30 kuanzia sasa huku kundi kubwa likilengwa na kutajwa kuwa ni Taasisi za Serikali zikowemo za Elimu na Afya.

Haya yameazimiwa leo tarehe 23 Agosti, 2024 katika mkutano huu ambao umejumuisha wadau mbalimbali wakiwemo Waheshimiwa Madiwani, wakuu wa Divisheni, Vitengo, Kamati ya Usalama Wilaya na watendaji mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, huku Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kishapu akitoa wito na angalizo kwa Mkuu wa Shule au Mganga kwenye taasisi yake ambayo inadaiwa kuhakikisha inalipa madeni hayo haraka na vinginevyo atapaswa kujitathimini kama anatosha kwenye nafasi yake.

Awali akitoa taarifa ya RUWASA Wilaya ya Kishapu Injinia. Dickson Kamanzima amesema kuwa, moja kati ya jukumu lao kubwa ni kuhakikisha kuwa wanatoa huduma bora yenye kuwafikia wanachi kwa maji safi na salama wakati wote huku akitoa wito kwa wadau wengine kusapoti juhudi hizi kwakuwa wao peke yao hawawezi kulifanikisha hili kwani maji ni uhai.

Katika salamu zake Mwenyekiti wa mkutano huu ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kishapu amewaeleza wananchi kuwa Wadau wote wa mkutano huu wanalo jukumu kubwa la kuendelea kuelimisha jamii zetu katika maeneo tunayotoka juu ya matumizi sahihi ya maji safi na salama ikiwa ni pamoja kutunza vyanzo vya maji, kulipia ankara za maji kwa wakati na kuacha tabia ya kushawishi wananchi kuacha kuyatumia maji ya visima ili waweze kuletewa maji ya Ziwa Victoria kwani wakati ukifika maji hayo yatawafikia hata bila mgomo huu.

"Niwaombe wadau wote wa mkutano huu wa mwaka twende tukatekeleze jukumu hili muhimu la kuelimisha jamii tunayoishi nayo huko tunakotoka juu ya umuhinu wa matumizi sahihi ya maji safi na salama na pia watunze vyanzo vyote vya maji ili tuendelee kunufaika navyo," amesema 

Injinia Dickson Kamanzima akielezea jambo wakati wa mkutano wa wadau


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa