WADAU wa mazao ya dengu na choroko Mkoa wa Shinyanga kwa pamoja wameridhia kuanza kwa rasmi kwa matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi Ghalani huku wakiiomba Serikali kuendelea kutoa elimukwa wakulima na wafanyabiashara ili kuwa na uelewa wa pamoja katika utekelezaji wake.
Akitoa taarifa ya awali katika mkutano huu, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme amesema kuwa, ujio na uwepo wa mfumo huu wa Stakabadhi za Ghala una lengo la kumuwezesha mkulima na mfanyabiashara kuwa na tija katika shughuli zao huku akisisitiza juu ya usalama wa fedha zao kwakuwa zitakuwa chini ya Benki zetu.
RC MNDEME amesema kuwa, serikali haitakuwa tayari kabisa kuona mkulima au mfanyabiashara akidhulumiwa au kuonewa na upande wowote kwakuwa lwngo lake ni kuwakomboa wote kwa pmoja na wala siyo vinginevyo kama ambavyo imekuwa ikitafsiriwana baadhi ya makundi.
Ujio na uwepo wa Mfumo huu wa Stakabadhi za Ghala unakuja kuwa mwarobaini wa ubabaishaji katika utekelezaji wa shughuli za wakulima na wafabyabiashara ambao ni wanunuzi na wadau wakuu wa mazao haya," alisema RC MNDEME.
Kwa upande wake Naibu Mrajis Udhibiti, Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania Bw. Collins Nyakunga amesema kuwa, uwepo wa Mfumo wa Stakabadhi Ghalani ni utekelezaji wa Ilani ya CCM ha 2020 Ibara ya 34 (b), utekelezaji wa maelekezo na maono ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la kumtafutia soko la uhakika mkulima kupitia vyama vya ushirika.
Kuanza kwa utekelezaji wa mfumo huu kunatajwa kuchangia katika kuongeza uzalishaji wa mazao, kwani mkulima atapata fursa ya kuuza mazao yake kwa bei yenye faida, hivyo kuchochea wakulima kuongeza uzalishaji wa mazao kwa tija na ubora zaidi pamoja na kuongeza thamani ya mazao hayo.
HABARI PICHA
Mhe. Mboni Mhita, Mkuu wa Wilaya ya Kahama akifuatilia jambo wakati wa mkutano wa wadau wa mazao
Boma Street, Mwanza Road
Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga
Simu: +255 28 2762222
Simu ya Mkononi:
Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz
Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa