• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Wadau watoe elimu kuwazuia vijana kufanya ngono, siyo matumizi ya kondomu

Posted on: February 1st, 2019

Wadau watoe elimu kuwazuia vijana kufanya ngono, siyo matumizi ya kondomu

Wadau wa masuala ya afya na uzazi wamesisitizwa kutoa elimu zaidi ya kuwataka vijana kuepuka kufanya ngono katika umri mdogo, badala ya kuwasisitiza kutumia kondomu na njia nyingine za uzazi wa mpango.

Akizungumza na washiriki wa warsha ya kufunga mradi wa “DREAMS’ uliotekelezwa kwa miaka miwili na shirika la “amref health Africa” katika Mkoa wa Shinyanga, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amesema ni vema wadau wawe pamoja na Serikali katika kuwajengea uzalendo watoto.

“Suala la kutumia vizuizi si salama sana, watoto wadogo waachane na ngono utotoni wanakimbilia wapi? Hebu tujikite kwanza kuwataka hawa watoto waache ngono utotoni. tunapotoa njia hizi tukaona wanazikimbilia tunakuwa tunafungua milango ya zinaa, muda wao bado” Amesema Telack.

Amesisitiza kuwa vijana wenye umri wa miaka 15 – 16 bado ni wadogo sana.

Amewataka pia Watumishi wa vituo vya Afya pia wakiona watoto hao wanakwenda kutafuta kinga wawaulize ili wanaume wanaowarubuni wakamatwe kwani hata dini zinakataza kujiingiza kwenye ngono katika umri mdogo.

Amesema wengine wakipata njia hizi wanaenda kufanya ngono zembe, matokeo yake hatuwezi kupunguza maambukizi ya VVU. Walimu waseme na watoto wa kike waache kujiingiza kwenye vishawishi.

Hata hivyo amewapongeza shirika la “amref” waliofanya kazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, Wilayani Kahama kwa kuchangia pia kupanda kwa ufaulu wa mtihani wa kidato cha nne mwaka jana ambapo Mkoa umeshika nafasi ya tatu kutoka nafasi ya nne mwaka 2017.

Aidha, Mhe. Telack ametumia pia nafasi hiyo kuwaomba waone sababu ya wao kubaki kufanya kazi Mkoani hapa na kupanua wigo katika Halmashauri nyingine.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa