• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WAFANYABIASHARA, ONGEZENI UTAYARI NA UHIARI WA KULIPA KODI - RC MACHA.

Posted on: March 1st, 2025

Na. Paul Kasembo, KAHAMA DC.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ametoa wito kwa wananchi kiongeza utayari na uhiari wa kulipa Kodi huku akiwasisitiza watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuendeleza uaminifu, uzalendo na ufanisi zaidi katika utekelezaji wao wa majukumu ili kuendelea kufikia lengo lao kwa mwaka pasipokuwa na malalamiko na kero kwao jambo ambalo litawapelekea wafanyabiashara kuwa na ukaribu sana na TRA.

RC Macha ameyasema hayo wakati akiongoza Hafla ya Utoaji Tuzo ya Mlipa Kodi kwa mwaka 2023/2024 zilizofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Malex ulipo Manispaa ya Kahama na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita, Meneja TRA Mkoa wa Kikodi Shinyanga ndg. Emmanuel Maro na Meneja wa TRA Mkoa wa Kikodi Kahama ndg. Warioba Kanire, wafanyabiashara na wananchi.

"Wafanyabiashara, niwaaombe sasa muongeze utayari na uhiari katika kulipa kodi ili Nchi iweze kusonga mbele kimaendeleo na kuwaletea huduma zote stahiki wananchi, nanyi TRA endelezeni uaminifu, uzalendo na ufanisi zaidi katika utekelezaji wa majukumu yenu katika kuwahudumia wananchi ili muendelee kufikia lengo kusudiwa pasipokuwa na malalamiko wala kero kutoka kwa wafanyabiashara jambo ambalo litawapelekea wqo kuwa karibu na TRA, amesema RC Macha.

Aidha, ameongeza kwa kusema kuwa yeyote yule asiyetoa stakabadhi kwa mnunuzi anayenunua bidhaa na yjle asiyedai wala kuchukua stakabadhi kutoka kwa muuzaji wote hao wanakuwa wanalihujumu Tiafa na siyo wapenda maendeleo kwani kila mmoja akitekeleza wajibu wake anakuwa anasaidia maendeleo kwa Taifa na kuinua uchumi wa wananchi wote kwakuwa mapato yataingia Serikalini na hivyo kupelekea lengo kuu la kufukiwa ambalo ni kuwapelekea maendeleo na huduma zote muhimu wananchi na kujenga imani kubwa wa Serikali yao.

Akitoa salamu za Mamlaka kwa niaba ya Kamishna wa TRA Tanzania ndg. Emmanuel Nnko ambaye pia ni Mkurugenzi wa TEHAMA TRA - Kahama alisema kuwa hafla hiyo ni kielelezo cha kutambua, kuthamini na kuheshimu mchango mkubwa wa walipa kodi kwa Mkoa wa Kikodi Kahama na Shinyanga.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa