• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Serikali yawataka Wafanyabiashara Shinyanga kuchangamkia fursa za ujenzi wa Bomba la Mafuta

Posted on: July 4th, 2019

Wafanyabiashara wa Mkoa wa Shinyanga na Mikoa jirani wametakiwa kujipanga na kuchangamkia fursa za uwekezaji katika mradi wa bomba la mafuta ghafi Afrika Mashariki hususani kwenye maeneo yatakayopitiwa na bomba hilo linalojengwa kutokea nchini Uganda hadi Mkoani Tanga.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge,kazi, vijana, ajira na watu wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na wadau zaidi ya 100 walioshiriki warsha ya kujadili fursa za ushiriki wa Watanzania katika mradi huo, iliyofanyika mwanzoni mwa wiki hii Mkoani Shinyanga, amesema bomba hilo litapita ndani ya Mikoa 10 ya Kagera, Mwanza, Geita, Shinyanga, Mara, Tabora, Singida, Manyara, Arusha, Tanga na Simiyu na litawanufaishwa Watanzania wote hasa wa Mikoa hii.

Mhe. Mhagama amesema Serikali inatekeleza Sera na miongozo iliyowekwa kwa lengo la kuwawezesha wananchi kiuchumi hivyo bomba hili ni moja ya miradi ya kimkakati kati ya miradi mikubwa Nchini na utatumia tekinolojia mpya katika sekta ya mafuta.

Mhagama amesema kuwa, warsha hiyo ya siku mbili ambayo itafanyika pia katika Mikoa hiyo 10 itawasaidia wadau kujifunza fursa zitakazojitokeza wakati mradi huu utakapoanza kujengwa hadi kukamilika kwake na ndiyo sababu Baraza la uwezeshaji wananchi kiuchumi limeamua kupita kwenye Mikoa hii. 

Amewataka wataalamu kufanya utafiti na kuhakikisha kuwa, Watanzania wote wanapata habari sahihi kuhusu fursa zitakazopatikana ili ziweze kufanyiwa kazi katika ubora na viwango vinavyotakiwa.

"Tumekubaliana kuwa, kupitia dira ya Taifa na mipango mbalimbali ya maendeleo kufikia mwaka 2025, sasa ni wakati wa Watanzania kuamka na kuyafahamu mambo mazuri yanayofanywa na taifa lao, miradi mikubwa inayotekelezwa na kwa kiasi gani ina uwezo wa kuwashirikisha waz kutumia fursa ya kuwaendeleza kiuchumi" amesema Mhagama

Naye Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amewahimiza Wafanyabiashara kujipanga sasa kuwekeza kwenye Mkoa kwani mradi huu utakuwa na fursa nyingi sana, "tuhakikishe fursa zinazokuja kwenye bomba la mafuta zisiwe changamoto kwenu, mjipange kuhakikisha mnainuka kiuchumi"

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa