Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Wafungwa 74 Shinyanga waachiwa kwa msamaha wa Rais Magufuli

Posted on: December 10th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amewataka wafungwa walioachiwa gerezani kwa msamaha wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Magufuli kubadilika na kuacha uhalifu watakapokuwa uraiani.

Akizungumza na baadhi ya wafungwa hao kati ya wafungwa 74 walioachiwa kwa Mkoa mzima mapema leo tarehe 10/12/2019 katika Gereza la Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Telack amewaasa kutorudia makosa yaliyowapeleka gerezani vinginevyo wakirudi tena hawatapata msamaha huo.

"Anachoamini Rais ni kuwa mmejutia makosa mliyoyafanya, ni matarajio yetu leo mmetoka mnaungana na familia zenu, muache kufanya uhalifu" amesema Telack.

Amewasisitiza kwenda kufanya kazi zinazowawezesha kuishi ikiwemo kilimo hasa wakati huu wa mvua pamoja na kuwa na hofu ya Mungu.

Nao baadhi ya wafungwa waliopata msamaha wa Rais wamemshukuru Mhe. Rais Magufuli na kuahidi kuwa raia wema wanaporudi uraiani.

Akitoa taarifa ya wafungwa walioachiwa, Afisa Magereza wa Mkoa Kamishna Msaidizi Wilson Rugamba amesema kuwa katika magereza yaliyopo Mkoani ya Shinyanga ambayo ni gereza la Shinyanga na Gereza la Wilaya ya Kahama, walioachiwa kwa msamaha wa Rais ni wafungwa 74.

Mhe. Rais Magufuli ametoa msamaha huo kwa zaidi ya wafungwa 5000 hapo jana tarehe 09/12/2019 wakati akitoa hotuba ya maadhimisho ya siku ya Uhuru ambayo ni idadi kubwa ya wafungwa kupata msamaha huo.

Baadhi ya Wafungwa wa Gereza la Shinyanga walioachiwa kwa msamaha wa Rais

"Rais anaamini mmejutia makosa yenu badilikeni fanyeni kazi, huko nje zipo kazi nyingi za kuwawezesha kuishi ikiwemo kilimo" Mhe. Telack

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa