Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WAJIRI SIMAMIENI STAHIKI ZA MAKATIBU MAHSUSI

Posted on: December 8th, 2023

Na. Shinyanga RS

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme amewaagiza waajiri wote ndani ya mkoa wa shinyanga kuhakikisha wanasimamia stahiki zote za makatibu mahsusi huku akisisitiza kuwa yeyote anayewabeza na kuwadharau makatibu mahsusi huyo hajitambui.

Agizo hilo amelitoa leo tarehe 7 Desemba, 2023 wakati akifungua kikao kazi cha kuzindua Chama cha Makatibu Mahsusi (TPSEA) mkoa wa Shinyanga mara baada ya kupokea risala ya wanachama hao ambapo ndani yake ilielezea changamoto mbalimbali ikiwemo kukosa stahiki zao kama kuhudhuria mafunzo na mikutano mbalimbali inayohusu taaluma yao.

"Nimesikiliza  kwa makini risala yenu nichukue nafasi hii kuwaagiza waajiri wote kusimamia stahiki za makatibu mahsusi ikiwemo kutenga bajeti ya kuhudhuria mafunzo na mikutano mbalimbali inayohusua taaluma yao pamoja na kuwapatia ruhusa ya kushiriki mafunzo na mikutano hiyo huku akimuagiza Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Prof. Siza Tumho kusimamia utekelezaji wa maagizo haya." amesema Mhe. Mndeme

Aidha, Mhe. Mndeme ameendelea kusisitiza kuwa makatibu mahsusi ni watu muhumu sana katika ofisi wanabeba siri nyingi pamoja na kujua mambo mengi yanayohusu ofisi, mtu akiwadharau makatibu mahsusi basi mtu huyo atakuwa hajitambui.

Pamoja na mambo mengine Mhe. Mndeme amewasihi makatibu mahsusi kupata muda wa kujiendeleza vizuri kielimu ili wawezi kuwa viongozi mbalimbali Kitaifa

Chama cha Makatibu Mahsusi (TAPSEA) kina jumla ya wanachama 118 kutoka Taasisi za Serikali na umma Mkoani Shinyanganga.

HABARI PICHA

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa