• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

Posted on: February 11th, 2025

KATIBU Tawala Mkoa wa Shinyanga CP. Salum Hamduni akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha, amewaomba Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga kutumia taaluma zao kuisaidia hospitali kukamilisha miradi ya ujenzi kwa haraka ili kuleta tija na kuwasaidia wananchi kupata huduma bora.

CP. Hamduni ameyasema haya leo Februari 11, 2025 wakati akizindua Bodi ya Ushauri ya Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Shinyanga, kikao kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Vigimark ambapo pamoja na yote amewapongeza wajumbe wote kwa kuteuliwa na Waziri mwenye dhamana ya Afya na kuwataka kutimiza majukumu yao kwa bidii.

“Ninawapongeza wajumbe wote kwa kuteuliwa kwenu na ninawaomba sasa mkatumie vema taaluma zenu ili kuisaidia Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga na kukamilisha miradi ya Ujenzi kwa haraka ili kuleta tija na kuwasaidia wananchi kupata huduma bora zaidi, lakini pia itasaidia kuongeza makusanyo ya fedha bila kuathiri huduma kwa wananchi” amesema RAS CP. Hamduni

Akizungumza kwenye uzinduzi wa bodi hiyo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Shinyanga Daktari Luzila John amesema Hospitali hii inatarajia kuwa na jumla ya majengo 25 ili kukidhi utolewaji wa huduma mbalimbali zenye hadhi ya Hospitali ya Rufaa.

Aidha Makamu Mwenyekiti wa Bodi Daktari John Majigwa pamoja na mambo mengine ametoa shukrani kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi hiyo Ndg. John Majiko ameahidi kuwa watafanya kazi kwa uwezo na weledi wao wote, nguvu zao zote na kwa bidii ili kukamilisha miradi ya ujenzi na kuinua huduma za afya za hospitali.

Uwepo wa Bodi ya Ushauri katika Hospitali ya Mkoa unatajwa kwenda kuongeza tija, kuboresha na kuongeza usimamizi wa karibu katika utoaji wa huduma kwa wananchi na kwa watumishi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga jambo ambalo litapekea kuongezeka pia kwa mapato ya kwa Hospitali na Serikali kwa ujumla.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa