• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Wakulima watakiwa kumiliki Vyama vya Ushirika

Posted on: August 14th, 2017

Wadau wa Ushirika Mkoa wa Shinyanga wamewataka wakulima kutambua kuwa umiliki wa vyama vya ushirika ni wa wakulima wenyewe na siyo Serikali.

Wakijadili katika kikao cha pamoja cha wadau wa ushirika Mkoa, kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wadau hao wamesema changamoto kubwa inayoua vyama vya ushirika ni wanachama wa vyama hivyo kutotambua umiliki wao.

Wamesema ifike mahali wanachama wajue kuwa ushirika una wenyewe.

Mwenyekiti wa chama kikuu cha ushirika cha KACU Bw. Emmanuel Charahani amesema changamoto kubwa ni kutobadilika kwa uongozi kwenye vyama vingi vya ushirika kwa muda mrefu hivyo wenyeviti na mameneja hao kuwa kama watemi kwenye maeneo husika na matokeo yake wanachama wanashindwa kutambua umiliki wao.

Awali, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na uzalishaji Bw. Dotto Maligisa alisema kuwa vyama vya ushirika ni moja ya vikundi vinavyowezesha wananchi kiuchumi ndiyo sababu ya kujadili ili kuinua uchumi wa nchi.

Akitolea mfano wa zao la pamba, Bw. Maligisa amesema nchi nyingi Duniani zimekuza uchumi kutokana na viwanda vya nguo ambapo asilimia kubwa ya nguo tunazovaa zinatokana na zao hilo hivyo, Mkoa wa Shinyanga kwa kuwa ni kati ya Mikoa inaongoza kwa kilimo cha Pamba una dhamana kubwa ya kuhakikisha unainua zao hili kupitia Wakulima ambao ndiyo wanachama wa ushirika.

Katika kikao hicho kilichoongozwa na Kaimu mrajis wa vyama vya ushirika Mkoa wa Shinyanga Bibi Shose Monyo, maazimio mbalimbali yamewekwa yenye lengo la kuinua ushirikia, ikiwemo kuhakikisha usimamizi kwa wakulima wenyewe kupitia vyama vyao vya msingi na vyama vya ushirika waweze kujitambua na kumiliki vyama hivyo.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa